• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

“Asiyetaka kupunguza mifugo yake ahame, hatutaki kupoteza Ziwa Rukwa,” RC Wangabo.

imewekwa Tar: November 16th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameiagiza kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya inayoongozwa na Mwenyekiti wake Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga kuhakikisha wanashirikiana na Halmashauri kupunguza idadi ya mifugo iliyopo kwenye halmashauri hiyo ili kudhibiti utunzaji wa vyanzo vya maji pamoja na hifadhi za misitu na kuliokoa ziwa Rukwa.

Amesema kuwa shughuli hizo za ufugaji karibu na vyanzo vya maji ndizo zinazopelekea kujaa kwa tope katika ziwa Rukwa, ziwa linaloasisi jina la Mkoa huo na kuongeza kuwa serikali haipo tayari kuona ziwa hilo likipotea na kusisitiza kuhifadhiwa kwa namna yoyote ile ikiwemo kupiga marufuku kufanbya shughuli za ufugaji kwenye vyanzo vya maji.

“Nashkuru kwamba zoezi la kupiga chapa linaendelea ila baada ya kumaliza zoezi hilo muanze kwenda boma kwa boma muhakikishe kwamba animal Unit “idadi ya mfugo kwa eneo” inazingatiwa, mtu ashauriwe kupunguza mifugo yake au ahame akatafute mahali pengine, kwasababu hatuwezi kujaza mifugo kwenye bonde la ziwa Rukwa halafu ziwa likafutika, serikali haitakubali.” Alibainisha.

Ameyasema hayo baada ya kusomewa taarifa ya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga katika Ziara yake ya siku mbili yenye lengo la kutembelea miradi mbalimbali, kujitambulisha kwa watumishi pamoja na kuongea na makundi mbalimbali ya wananchi katika halmashauri hiyo.

Katika taarifa hiyo ilionesha kuwa idadi ya wanyama iliyopo katika bonde hilo ni 143,346 huku idadi inayotakiwa ni 36,666 huku ikionesha kuongezeka mara tatu zaidi ya mahitaji ya uwepo wa Wanyama hao katika bonde hilo.

Katika kulisisitiza hilo Mh. Wangabo amewatahadharisha wananchi kufuga kisasa kwa kuwa na mifugo michache yenye kuleta tija huku ikizingati uhitaji wa ardhi kwaajili ya kilimo na shughuli nyingine za kibinaadamu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa skimu ya umwagiliaji Kijiji cha Ng’ongo, kata ya Mtowisa Wilayani Sumbawanga, Justin Amon amesema kuwa wafugaji wamekuwa wengi katika bonde hilo hasa katika skimu yao hiyo na kuwasababishia hasara pale wanapopeleka mifugo yao kwaajili ya malisho.

“Kama taarifa ilivyosomwa wafugaji wapo wengi ambao wamegeuza eneo hili kuwa sehemu ya machungio, tunapojaribu kuwafuatilia wanatushishia na mawe, fimbo, sime na mapanga na wapo tayari kupambana kwa lolote litakalotokea, na kesi zipo mahakamani lakini  tunaambiwa hatujakamilisha vigezo, hivyo tunashindwa na kushindwa kujua kwamba tunasaidiwaje na serikali yetu, wafugaji wanatunyanyasa sana,” Alisema.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA - 2025, KULINGANA NA MATOKEO YALIYOTANGAZWA NA BARAZA LA MITIHANI LA TAIFA (NECTA) June 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO ATEMBELEA FORODHA YA KASESYA, AHAMASISHA UWEKEZAJI

    July 15, 2025
  • RC MAKONGORO AFUNGUA JENGO JIPYA LA TAWI LA TCB SUMBAWANGA, APONGEZA KUIMARIKA KWA HUDUMA ZA KIFEDHA.

    July 10, 2025
  • UFAULU KIDATO CHA SITA; RUKWA YAZIDI KUPAA, RC MAKONGORO APONGEZA

    July 10, 2025
  • SERIKALI YAPIGA MARUFUKU TOZO ZA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    July 10, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa