• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

“Bila ya Ushirikiano kati ya TBA na SUMA JKT ofisi ya DC Kalambo haitakwisha kwa wakati” RC Wangabo

imewekwa Tar: January 25th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewasisitiza msimamizi mshauri wa ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kalambo ambao ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kushirikiana na Mkandarasi SUMA JKT kuhakikisha wanamaliza jengo hilo kwa wakati.

Amesema kuwa Ujenzi huo ulisimama zaidi ya miezi minne ambao ulitakiwa kumalizika mwezi wa 5 na kwa uchelewaji huo utasababisha kumalizika mwezi wa 10 jambo ambalo sio matarajio ya serikali ya awamu ya tano kufanya kazi kwa kusuasua.

“TBA wahakikishe wanashirikiana vizuri na SUMA JKT ili kumaliza ujenzi huu na ili hili jengo liende kwa kasi tunayoitaka kila mwezi tutakuwa tunapita kuangalia maendeleo ya ujenzi huo, sijaamini kwamba TBA wameshindwa kuwasimamia SUMA JKT ninachotaka makubaliano yote ya pande mbili yaheshimiwe ili kazi ziende kusiwe na mjuzi zaidi ya mwenziwe, mwelekezane” Mh. Wangabo alibainisha.

Hayo yamejitokeza baada ya Mh. Wangabo kutembelea ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kalambo na kuona kusuasua kwa ujenzi huo na kuamua kuitisha kikao ili kujua sababu za kujitokeza kwa hali hiyo ambayo sio makubaliano na hakuna taarifa za kuridhisha juu ya maendeleo ya ujenzi huo.

Awali akitoa taarifa ya kusuasua kwa ujenzi huo Meneja wa Wakala wa Majengo Mkoa wa Rukwa Arch Deocles Alphonce amesema kuwa ujenzi huo ulitakiwa kumalizika tarehe 16/5/2018 lakini kutokana na sababu za hali ya hewa na mabadiliko ya ramani kutokana na jiografia ya eneo ndio iliyopelekea kuchelewa kwa ujenzi huo kumalizika kwa wakati.

Nao Suma JKT wakimshukuru Mh. Wangabo kwa kuwakutanisha makundi matatu, wao kama Mkandarasi, Mteja ambae ni ofisi ya Katibu Tawala mkoa pamoja na Msimamizi Mshauri (TBA) kuelekezana palipokwenda tofauti na hatimae kufikia muafaka na kuendelea na ujenzi huo wenye thaamni ya Shilingi Milioni 289.

 

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waliokula Shilingi Milioni 932 za Halmashauri kufikishwa mahakamani.

    February 24, 2021
  • Wajumbe RCC waiomba Serikali kuhuisha Mradi wa VETA Sumbawanga ili kuwakomboa Wananchi.

    February 23, 2021
  • Shughuli za kibinadamu bado ni Changamoto katika uharibifu wa madaraja na barabara

    February 22, 2021
  • SITA WAFA KWA MATUKIO TOFAUTI IKIWEMO RADI

    February 18, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa