• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

DC Nkasi aonya wanaotishia hali mbaya kiuchumi.

imewekwa Tar: November 7th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda amewaonya wale wote wanaowatia hofu wananchi wa mwambao wa ziwa Tanganyika juu ya ugumu wa maisha baada ya kufanyika oparesheni ya kukamata wavuvi haramu katika mwambao huo.

“kuna kikundi kidogo cha watu kazi yao kuwajaza wananchi hofu, baada ya suala la (operesheni ya) Samaki kuanza tulipokea kama simu sita saba hivi wengine wakitoka hapa kirando, tukafuatilia, tukawaita wale maafisa wanaofanya oparesheni, tukakaa nao, tulikuwa tunaambiwa huruhusiwi hata kusafirisha samaki hata kama ni mmoja, tukajua hali ni mbaya, tuliuliza nia ya operesheni tukaambiwa ni kudhibiti uvuvi haramu sio kuzui biashara ya samaki,” Alisema.

Ameyasema hayo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wavuvi hao walizozielekeza  kwa Mkuu wa Mkoa akiwa ziara fupi kata ya kirando ili kujionea maafa yaliyotokea siku chache zilizopita yalisababishwa na mvua kali na kuharibu nyumba 27 na kutia hasara ya shilingi milioni 26.

Ameongeza kuwa wavuvi hao walikuwa wanalalamika kutozwa kuanzia milioni tano kama faini ya kukiuka sheria za uvuvi lakini baada ya mkuu wa Wilaya huyo kutangaza aliyetozwa kiasi hicho ajitokeze ili arudishiwe fedha yake, hakutokea hata mwananchi mmoja.

Aliwataka watu kuacha hofu na wengine kuacha kuwapa wenzao hofu kwa kuwaambia kuwa shughuli za uvuvi hivi sasa hakuna na kwamba watu wanaotegemea shughuli hizo watalala na njaa jambo ambalo si la kweli.

Mmoja wa wavuvi hao Ali Seif alisema kuwa wavuvi wamekuwa wakitozwa faini kubwa kuliko kawaida ikiwemo faini ya shilingi milioni tano na milioni kumi huku mvuvi mwingine Rashid Huseni aliongeza kuwa wakazi wa Kijiji cha Kirando kwa asilimia 99 wanategemea ziwa Tanganyika kwaajili ya vipato vya vya kuendesha maisha hivyo operesheni hiyo inawakosesha vipato hivyo na kusababisha watu wajiingize kwenye uhalifu.

Akitoa maelekezo ya Serikali katika utekelezaji wa zoezi hilo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alisisitiza kuwa aliapa kuitetea na kuilinda sheria ya nchi na hana mpango wa kwenda kinyume na sheria ambayo ilishapitishwa ila ataendelea kusisitiza utekelezaji wake hadi hapo itakapobadilishwa na vyombo husika.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa