• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Halmasahuri Mkoani Rukwa zatenga milioni 79 kununua mbegu za kahawa.

imewekwa Tar: October 10th, 2018

Zao la kahawa ni miongoni mwa mazao matano ya biashara ambayo serikali ya awamu ya tano imeamua kwa dhati kutilia mkazo uzalishaji wake, kwa mkoa wa Rukwa zao hilo ndio zao ambalo limeonekana kustawi kwenye baadhi ya maeneo na kupelekea halmashauri za mkoa huu kutenga shilingi milioni 79 kwaajili ya kununua mbegu ili kuendeleza zao hilo.

Mkuu wa Mkoa wa rukwa Mh. Joachim Wangabo amesema kuwa kama mkoa hatuna budi kutilia mkazo uanzishaji na uendelezaji wa zao hili ili wakulima wetu waweze kuwa na zao la biashara na kubainisha kuwa tayari maeneo kwaajili ya kilimo hicho yameshabainishwa ambapo makampuni, taasisi na wakulima wameonyesha nia ya kulima.

“Eneo la kiasi cha ekari 3,195.83 limebainishwa kwa ajili ya kulimwa zao la kahawa. Jumla ya wakulima 2,266 na taasisi 9 zitajihusisha katika uzalishaji wa kahawa. zikiwemo taasisi za Jeshi la Magereza pamoja na Jeshi la Wananchi Tanzania.”Alisema.

Ameyasema hayo katika kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC) kilichofanyika mwezi huu wa nane katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa Mkoa ikijumuisha wadau mbalimbali wa maendeleo, Wabunge, Madiwani, Viongozi wa dini na wataalamu wa Halmashauri na sekretarieti ya mkoa.

Aidha, mbunge wa viti maalum Mkoa wa Rukwa Mh. Aida Khenan amesema kuwa kilimo cha kahawa kinahitaji wakulima wenye uwezo wa kifedha ambao katika mkoa wa rukwa wakulima hao hawapo na kusisitiza kuwa wakulima wa mkoa huo wamezoea kilimo cha muda mfupi.

“kahawa inahitaji fedha na muda, wakulima wetu wamezoea kilimo cha muda mfupi, watakaoweza kumudu kahawa ni wale wenye uwezo, masuala ya madawa na kuhudumia hiyo kahawa, wataalamu wetu wafanye utafiti watuambie zao lipi la kibiashara litaleta tija kwa wananchi wetu hasa katika msimu huu wa kilimo,” Alisema.

Mh. Wangabo alieleza kuwa mkoa umejipanga katika kuhamasisha kilimo cha zao la alizeti kama zao la kibiashara kwani hali ya uzalishaji wa zao hilo kwa sasa hairidhishi na hivyo kutoleta tija kwa wakulima.

“Hali ya uzalishaji wa zao la alizeti katika Mkoa umebaki kuwa ni wastani wa gunia  6.5 za kilo 65  kwa ekari sawa na  tani 1.1 kwa hekta. Tija hii ni ndogo sana ukilinganisha na tija iliyofanyiwa utafiti ya gunia 12-16 kwa ekari ambazo ni sawa na zaidi ya tani 2.00 kwa hekta.” Alibainisha.

Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kutilia mkazo uzalishaji wenye tija wa mazao matano ya biashara ambayo ni Korosho, Chai, Kahawa, Tumbaku na Pamba.

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • UTARATIBU WA UOMBAJI WA VITAMBULISHO VYA UJASILIAMALI March 24, 2021
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara waombwa kuwa na huruma na wanaofunga mwezi wa Ramadhan

    April 16, 2021
  • Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

    April 15, 2021
  • Mwamko mdogo wa Wananchi wakwamisha zoezi la Urasimishaji Makazi Sumbawanga

    April 14, 2021
  • Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

    April 05, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa