• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Hospitali za Wilaya 67 zafanyiwa tathmini juu ya maenedeleo ya ujenzi wake.

imewekwa Tar: December 19th, 2019

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamuhanga amesema kuwa  Ofisi ya Rais inaendelea kufanya tathmini kwa hospitali zote 67 kuhakikisha kwamba shilingi bilioni 100.5 ambazo zilitolewa kwa ujenzi wa hospitali hizo kuwa zimetumika vizuri.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imejenga hospitali 67 nchini na mkoa wa Rukwa umejengewa hospitali tatu za wilaya ambapo Mhandisi Nyamuhanga aliweza kutembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Kalamnbo, katika mji mdogo wa Matai iliyopokea shilingi Bilioni 1.5 lakini hakuridhishwa na ujenzi wa hospitali hiyo.

 “Kwa halmashauri ambazo fedha hizi zitakuwa hazijatumika vizuri kwakweli tutachukua hatua na katibu tawala wa mkoa kama nilivyoagiza jana, najua kuna vifaa ambavyo tayari vimeshanunuliwa pale ambavyo bado havijawekwa, havijajengwa kwa mfano maru maru na vifaa vingine uhakikishe kwamba kazi hiyo inaendelea ili vifaa hivyo vikishawekwa tuvitathmini sasa kiwango cha ukamilishaji wa hospitali ile ya halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kabla hatujafikiria kutoa fedha nyingine za kukamilisha,” Alisema.

Ameongeza kuwa halmashauri hiyo ya Kalambo imetaja mahitaji ya shilingi milioni 700 ili kuweza kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo jambo ambalo Mhandisi Nyamuhanga hakukubaliana nalo kutokana na tathmini iliyofanywa ya mahitaji ya fedha walizotoa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hizo kuwa yangebaki mambo machache ambayo yasingeweza kuzidi shilingi milioni 300 na kuongeza kuwa anahitaji maelezo ya ziada kutoka katika halmashauri hiyo ambayo hospitali yake imefikia ukamilifu wa asilimia 76 ambacho ni kiwango cha chini cha ukamilishaji.

Katika hatua nyingine amesema kuwa mwezi Aprili mwaka 2019 Ofisi ya Rais TAMISEMI ilitoa shilingi milioni 400 kwaajili ya upanuzi wa Zahanati ya Kijiji cha Samazi katika halmashauri ya Wilaya ya Kalambo ambapo zahanati hiyo inapandishwa hadhi na kuwa kituo cha Afya lakini amesikitishwa na malumbano yanayoendelea katika kijiji hicho juu ya eneo la ujenzi wa kituo hicho jambo lililopelekea kushindwa kuanza kwa ujenzi huo.

“Ofisi ya Rais TAMISEMI imetoa maelekezo kwamba upanuzi ufanyike katika eneo la zahanati iliyopo iongezewe majengo ili kiwe kituo cha afya cha Samazi kiweze kukamilika ili kiweze kufanya kazi, tusiendelee na malumbano tena tumeshatoa maamuzi kwamba upanuzi ufanyike pale kwenye zahanati ili tukipandishe hadhi ikiwe kituo cha afya, tunategemea kazi hiyo ianze mara moja na ikamilike ndani ya miezi mitatu,” Alisisitiza.

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • UTARATIBU WA UOMBAJI WA VITAMBULISHO VYA UJASILIAMALI March 24, 2021
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara waombwa kuwa na huruma na wanaofunga mwezi wa Ramadhan

    April 16, 2021
  • Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

    April 15, 2021
  • Mwamko mdogo wa Wananchi wakwamisha zoezi la Urasimishaji Makazi Sumbawanga

    April 14, 2021
  • Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

    April 05, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa