• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Jimbo Katoliki la Sumbawanga lazindua jengo la Wagonjwa wa nje wa Macho

imewekwa Tar: October 24th, 2020

Katika kusaidia juhudi za serikali kuboresha huduma katika mkoa wa Rukwa, Jimbo Katoliki la Sumbawanga kwa ufadhili wa Shirika la German Committee for Prevention of Blindness (DKVB) limezindua jengo la wagonjwa wa nje wa macho katika hospitali teule ya Kumbukumbu ya Dkt. Atman mjini Sumbawanga ili kusogeza huduma kwa wagonjwa wa macho ambao awali walilazimika kusafiri umbali mrefu nje ya mkoa kufuata huduma hiyo.

Wakati akitoa taarifa fupi ya program ya macho kwa mikoa ya magharibi mwa Tanzania (Rukwa, Katavi na Kigoma) Msimamizi wa Mradi huo Ryner Linuma alisema kuwa tangu Novemba, 2017 shirika hilo lilipoanza kutoa huduma zake katika mkoa wa Rukwa kwa njia ya mkoba (Eye Care Surgical Outreach Camp) hadi Oktoba, 2019 jumla ya watu 4,296 walikuwa wamepatiwa huduma, ambapo 977 ka ti ya hao walifanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho, 526 walipatiwa miwani, 22 walipatiwa rufaa kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili na KCMC.

“Baada ya kuona idadi ya wahitaji wa huduma za macho kuwa kubwa na kuongezeka karibu kila kambi ya huduma ya macho inapofanyika, shirika liliona kuwa majuma mawili ya kambi hayatoshi na mfumo huu wa huduma za macho kwa mfumo wa Mkoba sio endelevu katika meneo haya, hivyo likaanza kufikiria namna ya kufanya huduma hizi kuwa endelevu ndipo shirika liliposhirikisha serikali kupitia ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Jimbo Katoliki la Sumbawanga mwezi April,2019 na kufanya kikao,”

“Baada ya kikao hicho ikaanzishwa program maalum ya kuzuia upofu unaoweza kuzuilika katika mikoa ya magharibi mwa Tanzania kupitia utoaji wa huduma jumuishi za macho ikiwa na malengo ya kusomesha wataalamu waajiriwa wa Serikali na Jimbo Katoliki katika ubobezi wa utoaji wa huduma za macho, Kujenga jingo maalum la huduma za macho na vifaa tiba na kuendeleza mahusiano baina ya sekta binafsi na umma katika kutoa huduma endelevu za macho ndani ya Mkoa,” Alielezea.

Kwa upande wake mgeni rasmi wa tukio hilo Mkuu wa mkoa wa Rukwa mh. Joachim Wangabo alisema kuwa anatambua na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na Jimbo Katoliki la Sumbawanga kusaidia juhudi za serikali za kuboresha huduma za afya katika mkoa ambapo kati ya vituo 239 vya kutolea huduma za afya ndani ya mkoa, vituo 21 vinamilikiwa na Jimbo Katoliki la Sumbawanga na kuongeza kuwa Hospitali ya Kumbukumbu ya Dkt. Atman ya Sumbawanga Mjini na Hospitali ya Namanyere Wilayani Nkasi zimekuwa zikitumika kama hospitali teule za halmashauri.

“Kabla ya kuhitimisha naomba nirudie tena kuwashukuru wadau wetu kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakitupatia kama serikali kupitia watumishi, vifaa na sasa jingo hili lenye thamani ya shilingi 343,888,580/=. Niwaombe wadau mnaohusika katika usimamizi wa huduma hizi kuhakikisha watumishi wote waliopatiwa mafunzo kupitia ufadhili huu wanatumika ipasavyo kuboresha huduma za macho katika mkoa kupitia kituo hiki na vituo vingine vilivyotajwa,” Alisisitiza.

Aidha Wakati akitoa neno la shukurani Mha. Baba Askofu Beatus Urassa wa Jimbo Katoliki la Sumbawanga aliwashukuru wafadhili pamoja na ushirkiano uliooneshwa na serikali katika kuhakikisha ujenzi wa jingo hilo unakamilika na wananchi wa Mkoa wa Rukwa na mikoa ya jirani wanapata huduma ambayo haijawahi kupatikana hapo awali.

“Kwa kadiri ninavyoufahamu mpango kazi wa Shirika hili la German Committee for Prevention of Blindness, makabidhiano haya na uzinduzi wa jengo hili la wagonjwa wa macho wa nje ni ngazi ya kuelekea mradi mkubwa Zaidi wa ujenzi wa Chumba cha upasuaji wa macho kuanzia muda wowote kabla ya mwaka 2021 na kutoa vifaa tiba pamoja na usafiri kwaajili ya program hii ya huduma za macho,”

Halikadhalika, Mwakilishi wa Shirika la German Committee for Prevention of Blindness Dkt. Karsten Paust aliishukuru serikali kwa ushirikiano uliopo katika kukamilisha azma hiyo ya kutoa huduma bora ya macho kwa wananchi wa mkoa wa Rukwa na mikoa ya magharibi mwa Tanzania.

Miongoni mwa mafanikio ya programu hiyo ni pamoja na kuwasomesha na kuwapatia vifaa tiba wauguzi 22 katika fani ya macho kutoka halmashauri nne za mkoa huo, kumsomesha mtaalamu mmoja wa miwani, kumsomesha daktari bingwa wa macho mmoja, kuwasomesha madaktari watatu wa upasuaji wa mtoto wa jichona kuanzisha mradi wa elimu ya afya ya macho katika halmashauri zote za mkoa.

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Waomba Daraja la muda baada ya watu wanne kuzama mtoni

    February 27, 2021
  • Wananchi walazimika kuzunguka Zaidi ya Km 30 kufuata huduma kwa kukosa barabara ya km 7.3.

    February 26, 2021
  • Helium Yaibuka Kikao cha Bodi ya Barabara na kuibua gumzo.

    February 25, 2021
  • Waliokula Shilingi Milioni 932 za Halmashauri kufikishwa mahakamani.

    February 24, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa