• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mkandarasi atakiwa kumaliza Jengo la Ofisi za Halmashauri kabla ya 2021.

imewekwa Tar: December 12th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkandarasi Suma JKT anayejenga Ofisi za halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kumaliza jengo hilo kabla ya mwaka mpya wa 2021 baada ya jengo hilo kudumu kwa miaka zaidi ya mitatu bila ya kukamilika.

Mh. Wangabo amesema kuwa Pamoja na kufahamu changamoto kadhaa za ujenzi zilizoikumba eneo hilo hali iliyofanya ujenzi wa msingi wa jengo hilo kuchukua muda mrefu kutokana na eneo hilo kujaa maji na hivyo mkandarasi kuomba kuongezewa muda wa kumalizia jengo hilo lakini ameongeza kuwa hatua hiyo imeshapita.

“Mkandarasi aliomba ‘extension’ kadhaa nay a mwisho inaisha tarehe 31 Disemba yam waka huu, sasa nikuangize mkandarasi uzingatie huo mkataba, mkataba huo wa tarehe hiyo niliyoisema ufuatwe, kazi zifanyike usiku na mchana, leo ni tarehe 11 bado kama wiki tatu, hili jingo linapaswa kukamilika vinginevyo tutatafakari hatua ya kuchukua kwasababu tumeshakaa muda mrefu miaka mitatu haikubaliki,” Alisema.

Aidha, alitahadharisha kuwa fedha inayotolewa kwaajili ya ujenzi wa jingo hilo kutumika kwaajili ya malengo ya ujenzi wa jingo hilo na sio badala yake Mkandarasi huyo kubadili matumizi ya fedha hizo kutokana na taratibu zao za kuweka fedha za miradi yao sehemu moja na hatimae kubadili matumizi.

Hata hivyo wakati akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi huo mshauri elekezi Kaimu Meneja Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Rukwa Mhandisi Haruna Kalunga amesema kuwa miongoni mwa changamoto wanazopata ni Pamoja na mshitiri kuchelewa kufanya malipo kwa wakati hali inayosababisha ucheleshwaji wa ujenzi huo.

“Kwa mfano hati ya madai namba 5 ilipitishwa na Mshauri Elekezi tarehe 5.6.2020 ila ilikuja kulipwa tarehe 5.10.2020 takriban miezi minne mkandarasi alikuwa anasubiria malipo, changamoto ya pili ni kuchelewa kupatikana kwa mkandarasi mdogo wa huduma, mpaka unaona jingo hili linaanza kutumika hadi leo halina miundombinu ya umeme,” Alieleza.

Ujenzi huo wenye thamani ya Shilingi 3,494,444,696/= unaojumuisha ujenzi wa vymba vya ofisi 137, jingo la mgahawa, uzio wa mita 427, kibanda cha mlinzi na maegesho ya magari ulianza tarehe 27.10.2017 na kutarajiwa kumalizika tarehe 25.5.2019 lakini hadi leo tarehe 11.12.2020 umefikia 56% huku mkandarasi akiwa amelipwa hati 5 za madai zenye jumla ya shilingi 1,869,535,687.55/= ambazo ni saw ana 45% ambapo gharama hizo ni bila ya kodi ya ongezeko la thamani (VAT).

Katika Hatua nyingine Mh. Wangabo amepongeza juhudi zinazofanywa na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kwa kutumia fedha zake za mapato kuendelea na ujenzi wa ofisi za halmshauri hizo wakati wakisubiri fedha kutoka serikalini lakini pia kuanzisha ujenzi wa Stendi ya Mabasi katika mji mdogo wa Laela ambao ndio makao makuu mapya ya Halmashauri hiyo baada ya agizo la Rais Mh. John Pombe Magufuli kuzitaka halmashauri hizo kuhamia katika maeneo yao ya kiutawala.

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waliokula Shilingi Milioni 932 za Halmashauri kufikishwa mahakamani.

    February 24, 2021
  • Wajumbe RCC waiomba Serikali kuhuisha Mradi wa VETA Sumbawanga ili kuwakomboa Wananchi.

    February 23, 2021
  • Shughuli za kibinadamu bado ni Changamoto katika uharibifu wa madaraja na barabara

    February 22, 2021
  • SITA WAFA KWA MATUKIO TOFAUTI IKIWEMO RADI

    February 18, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa