• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mvua Yakatisha Mawasiliano Mikoa ya Songwe, Rukwa na Katavi Huku Ikiua Watatu

imewekwa Tar: January 10th, 2020

Mvua zinazoendelea kunyesha katika mkoa wa Rukwa zimeendelea kusababisha maafa baada ya kusomba madaraja manne katika barabara ya Kasansa – Kilyamatundu inayounganisha mikoa ya Songwe, Rukwa na Katavi iliyopo bonde la ziwa Rukwa Wilayani Sumbawanga huku ikisababisha vifo vya watu watatu katika wilaya ya Kalambo na Nkasi mkoani humo.

Mvua hizo zilizosomba madaraja katika vijiji vya Muze, Kifinga, Lwanji na Msia vilivyopo Wilaya ya Sumbawanga imesababisha kukatika kwa mawasiliano baina ya kata na kata, kijiji na kijiji pamoja na mikoa hali iliyoleta taharuki kwa wananchi wanaoishi katika bonde hilo lenye kata 13 na wakulima wengi wa mpunga wanaosafirisha bidhaa zao katika mikoa ya jirani.

Aidha, Mvua hizo zimesababisha vifo vya Mama mjamzito na mwanawe kwa kusombwa na maji yam to Kalambo huko wilayani Kalambo na kifo cha mwanafuzi wa darasa la 4 mwenye umri wa miaka 12 katika Wilaya ya Nkasi ambae pia alisombwa na maji wakati akitoka shuleni kurudi nyumbani.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alipofanya ziara ya kutembelea maeneo yaliyokumbwa na maafa hayo na hivyo kuwatahadharisha wananchi kuacha tabia ya kulazimisha kupita katika njia ya maji pindi wanapoona mvua ni kubwa na hivyo kuwataka kusubiri mvua ipungue ndipo waendelee na shughuli zao.

“Mimi niwaombe ndugu zangu hasa kinamama na watoto, mnapoona mvua zimekuwa nyingi maji yanaweza yakajaa wakati wowote, jihadharini msipite, acheni maji yapungue halafu mpite, lakini msiwe wabishi, mkiwa wabishi mtabebwa na mafuriko, hasa watoto wadogo hawalelewi kitu wanadhani maji kama hivi anaona kama yametulia anasema mimi nitapita tu, kwahiyo waambieni watoto nyumbani wachukue tahadhari, mkiona kuna mvua kuna mafuriko watoto wasiende kwenye shughuli zao muwazuie kuokoa maisha yao” Alisisitiza

Na kuongeza kuwa hali hiyo si ya kudumu ni ya muda tu kwani serikali kupitia wakala wa barabara nchini TANROADS inaendelea na matengenezo ya dharura katika maeneo hayo ili kurudisha hali ya mawasiliano baina ya vijiji, kata pamoja na mikoa ili wananchi waendelee na shughuli zao za kila na hivyo kuwataka wakala hao kuweka kambi katika maeneo yaliyoharibiwa na mvua.

“Bonde la ziwa rukwa limeshakatika kimawasiliano kabisa kwasababu magari yanayotokea Mbeya, kule Somgwe kupitia daraja letu la Kilyamatundu pale hawawezi kufika Muze mpaka huko Katavi kama hapa hapatakuwa pameshughulikiwa kwahiyo weka nguvu kubwa sana Meneja wa TANROADS hapa ili kuhakikisha wananchi wetu wanapata usafiri wao wa kawaida ndani ya muda mfupi,”Alisema.

Kwa upande wake Meneja wa TANROADS mkoa wa Rukwa Mhandisi Masuka Mkina amesema kuwa tayari wamekwisha omba fedha za matengenezo ya dharura kutoka makao makuu na kuwataka wananchi kuacha tabia ya kufanya shughuli za kibinaadamu katika kingo za mito ili kuweza kuokoa miundombinu hiyo kuharibiwa na mafuriko.

“Nichukue nafasi hii kuwaomba viongozi wa vijiji na wengine watusaidie kwasababu sheria ya mazingira inasema wasifanye kazi karibu na mito na panapotukwamisha ni huko juu ambapo watu wanalima wanaharibu mazingira kwahiyo maji yanakuja kwa nguvu matokeo yake yanasomba miundombinu yetu na kutuacha kama hivi tukiwa wakiwa kabisa,” alisema

Kwa upande wao wananchi katika maeneo hayo waliiomba serikali kuharakisha matengenezo ya haraka kwani atahri wanayoipata ni kubwa katika upande wa kiuchumi na kijamii, miongoni mwa wananchi Erasmus Muhagama alisema, “Mi naiomba serikali iharakishe hili zoezi maana mawasiliano ndio yameshakatika”.

Nae Magdalena Tangi alisema, “Kwakweli kuna shida watu hawapiti safari zimekuwa ngumu, usafiri umekuwa wa pikipiki gharama kubwa kwahiyo wananchi tunapata shida sana kama hivi mlivyoona barabara zimekatika toka Muze mpaka hapa Msia sijui huko mbele sasa”.

Barabara hiyo Kasansa – Kilyamatundu yenye urefu wa kilomita 178 iliyopo kwenye bonde la ziwa Rukwa lenye kata 13 ni kiungo muhimu sana kwa kuunganisha mkoa wa Rukwa na mikoa ya Songwe na Katavi hasa katika shughuli za kiuchumi kwani asilimia kubwa ya wakazi wa bonde hilo ni wakulima wa mpunga, mahindi, alizeti pamoja na kufanya ufugaji. 

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waliokula Shilingi Milioni 932 za Halmashauri kufikishwa mahakamani.

    February 24, 2021
  • Wajumbe RCC waiomba Serikali kuhuisha Mradi wa VETA Sumbawanga ili kuwakomboa Wananchi.

    February 23, 2021
  • Shughuli za kibinadamu bado ni Changamoto katika uharibifu wa madaraja na barabara

    February 22, 2021
  • SITA WAFA KWA MATUKIO TOFAUTI IKIWEMO RADI

    February 18, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa