• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mwekezaji mwenye magunia 110,000 ya mahindi Rukwa atafutiwa soko.

imewekwa Tar: July 31st, 2018

Mkurugenzi wa shamba la Msipazi lililopo katiika kijiji cha China, kata ya Kate, wilayani Nkasi, Salum Summry ameiomba serikali kupitia ofisi ya mkuu wa mkoa wa rukwa kuona uwezekano wa kumtafutia soko la mahindi aliyovuna mwaka jana na mwaka huu ili kujiendeleza kibiashara.

Summry alisema kuwa tani 7200 za mahindi yaliyopo yamejaza maghala na hatimae mahindi yanayoendelea kuvunwa huwekwa nje jambo ambalo litahatarisha usalama wa mahindi hayo endapo mvua zitaanza kunyesha mwaka huu.

“Tunaiomba NFRA iweze kununua tani zaidi za mahindi maana yake mwaka huu wamenunu tani 5200 tu, tunaomba kutafutiwa soko, sisi peke yetu tuna tani 7200 kwenye maghala yetu na mengine tunaendelea kuvuna na kuyahifadhi hapo uwanjani kutokana na upungufu wa ma-godown (maghala), na mpaka sasa gunia 250 zimeharibika ila tutazigeuza kuwa pumba, hivyo hatutapata faida wala hasara,” Alisema.

Summry amesema kuwa wameona umuhimu wa kujaribu kupanda zao la alizeti katika ekari 1000 ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali ya Mkoa katika kuliimarisha zao hilo huku ekari 3200 akiwa amepanda mahindi.

Ametoa maombi hayo alipotembelewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa ikiongozwa na Mkuu wa mkoa Mh. Joachim Wangabo pamoja na Mkuu wa Wilaya hiyo na kamati yake ya Ulinzi ili kuona maendeleo ya mwekezaji huyo na kuona namna ya kufikisha huduma muhimu katika eneo hilo ambalo linatariwa kujengwa kiwanda cha mafuta ya alizeti, chakula cha kuku, pamoja na unga.

Mh. Wangabo alisema kuwa serikali ipo pamoja na wawekezaji katika kuhakikisha uchumi wa viwanda unafikiwa kwa asilimia 100 na kamwe haitawaangushga wawekezaji hao na kumtaka Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda kuwa karibu na mwekezaji huyo ili kuwezesha kusaidia kutimiza ahadi ya viwanda 100 kwa kila Mkoa.

“Nimeona kuna mlundikano mkubwa wa mahindi ya mwaka jana na mwaka huu, serikali ipo pamoja nawe katika kuhakikisha tunakupunguzia haya machungu, hivi karibuni Rais wetu alizungumza na shirika la WFP na wao wamesema kuwa wataongeza idadi ya kununua mahindi zaidi kutoka Tanzania, hivyo wasiliana na WFP kupitia NFRA ili nuwe wakala na kujihakikishia soko, lazima ujisajili nili uweze kuwasaidia na wakulima wengine kupata soko.”Alisema.

Pia Mh. Wangabo alitoa pongezi kwa mwekezaji huyo kwa kuunga mkono juhudi za mkoa katika kufufua zao la alizeti na kujenga bkiwanda cha mafuta hayo na kumuhakikishia kuwa kiwanda hicho kitapata malighali ya kutosha kutoka kwa wakulima wengine mkoani humo.

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • UTARATIBU WA UOMBAJI WA VITAMBULISHO VYA UJASILIAMALI March 24, 2021
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara waombwa kuwa na huruma na wanaofunga mwezi wa Ramadhan

    April 16, 2021
  • Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

    April 15, 2021
  • Mwamko mdogo wa Wananchi wakwamisha zoezi la Urasimishaji Makazi Sumbawanga

    April 14, 2021
  • Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

    April 05, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa