• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo azigeukia NGOs na CSOs kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda kupambana na umasikini

imewekwa Tar: March 27th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amezitaka asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali kuchukulia juhudi za uanziswaji wa viwanda nchini unaofanywa na serikali kama suala mtambuka na ukombozi kwa mwananchi katika kupambana vita dhidi ya Umasikini huku wakizingatia utunzaji wa mazingira na kushirikiana na SIDO.

Amesema kuwa takwimu zinaonesha kwamba takribani hekta 300,000 hadi 400,000 za misitu nchini huharibiwa kwa kuchoma Mkaa. Hivyo njia nyingine na muhimu kuokoa mazingira yetu ni kwa kuanzisha viwanda vya kutengeneza Mkaa kwa kutumia marando ya Mbao, Pumba za Mpunga, Mabua ya mahindi n.k. malighafi ambazo hupatikana kwa wingi Mkoani kwetu.

 “Kwa sababu hiyo ninapenda kutoa wito kwa NGOs na CSOs kushiriki kwenye kampeni hii ya uanzishwaji wa viwanda yenye kaulimbiu ya Mkoa wetu, Viwanda vyetu kwa kuanzisha viwanda. Viwanda tunavyovilenga ni vile vidogo vya thamani ya kuanzia milioni 2 hadi Milioni 10,” Alisisitiza.

Kwa upande wake Meneja wa SIDO Emanuel Magere amesema kuwa asasi pamoja na mashirika hayo yamekuwa yakitoa elimu mbalimbali kutegemea matatizo ama changamoto za wananchi lakini imefika wakati kutambua kuwa, wananchi hao wanahitaji pia elimu ya ujasiliamali ili kuanzisha viwanda, na kuziomba taasisi za fedha kuweza kutoa mikopo kwa wanaohitaji kuanzisha viwanda.

“Mwamko katika uazishwaji wa viwanda sio mkubwa sana, wengi wamekuwa wakijiwekeza kwenye sekta ya huduma mfano, mashule, migahawa, maduka na huduma mbalimbali ambayo “return” yake inakuwa ya haraka kuliko viwanda na pia changamoto ya masoko ya bidhaa za ndani ya mkoa kutoka kwa bidhaa za nje ya mkoa ama nje ya nchi imekuwa ni changamoto kwa mkoa,” Alimalizia.

Katika kuhimiza ushirikiano Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda amezitaka NGO na CSO hizo kuweza kufika kwenye ofisi za kiserikali ili kuweza kujitambulisha shughuli wanazofanya na kujitokeza kwenye songambele mbalimbali zinazofanywa na halmashauri katika ujenzi wa madarasa ya shule na vituo vya afya ili michango yao ijulikane na sio kusubiri kutafutwa na serikali.

Katika utekelezaji wa viwanda 100, ndani ya kipindi cha miezi minne kuanzia Disemba mwaka 2017 hadi 26, Machi, 2018 Mkoa wa Rukwa umezalisha viwanda vidogo 51 huku lengo la Mkoa ni kuwa na viwanda vingi zaidi ili kuchangia kwa kiasi kikubwa lengo la Kitaifa la kufikia nchi ya Uchumi wa Kati wa Viwanda ifikapo 2025.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa