• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi wasisitizwa kuitumia wiki ya sheria kama fursa ya mafunzo ya bure ya sheria.

imewekwa Tar: January 24th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi mkoani humo kuhakikisha wanafika katika mabanda ya kutolea elimu ya sheria ili kuitumia fursa ya kupata elimu hiyo inayotolewa bure kwa kipindi cha wiki nzima ya sheria.  

Mh. Wangabo amesema kuwa elimu hiyo inayotolewa na Mahakama Pamoja na wadau wengine ikiwemo Mawakili wa Kujitegemea, Serikali, Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa uendeshaji wa Mashataka (DPP), Ofisi ya Wakili (Solicitor General), Baraza la Ardhi Pamoja na Taasisi mbalimbali itawawezesha wananchi hao kuona njia za kutatua migogoro mbalimbali.

Amesema kuwa wananchi wamekuwa na malalamiko na migogoro mingi inayohusu mambo ya kisheria na hawajui sheria na hivyo kuwataka kuitumia wiki hiyo ya sheria iliyoanza tarehe 23.1.2021 kupata ushauri katika changamoto mbalimbali za kisheria wanazokabiliana nazo katika kutafuta haki zao.

“Elimu ni ya Bure itumieni hapa, kwa wale ambao watashindwa kufika hapa, wasikilize vyombo vya Habari, wasome magazeti, wafuatilie kule, kuna elimu ya bure ambayo inatolewa wiki nzima hii, tusikilize redio, watumishi wa mahakama wamejipanga, mahakimu majaji wanatoa elimu kule ya bure na wakati mwingine kutakuwa na mawasiliano ya moja kwa moja, unauliza swali lako utajibiwa.”

“Naona watu wengi sana wanamsumbua Mkuu wa Wilaya wakifikiri yeye ndio hakimu yeye ndio Jaji, yeye ndio mwanasheria, mtu anadhani akienda kule migogoro yake yote inaishia kule, sikilizeni fuatilieni vyombo vya Habari, ili muweze kujua masuala ya kisheria, si kila jambo linatatuliwa na mkuu wa Wilaya, Mkuu wa mkoa, Sisi tunafanya upatanishi ili watu waridhiane tu basi, lakini ukitaka haki ni mahakamani,” Alimalizia.

Mh. Wangabo ameyasema hayo wakati akifungua wiki ya sheria nchini leo tarehe 24.1.2021 kwa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga, wiki ambayo imeambatana na matukio ya kutembea umbali wa kilomita 9 pamoja na maadhimisho ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa Mahakama Kuu nchini.

Aidha, Mh. Wangabo ametumia nafasi hiyo kuipongeza Mahaka kuu ya Tanzania kwa kuadhimisha miaka 100 (karne moja) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1921 huku akiwashauri kutafakari kwa kina mambo yanayotakiwa kuboreshwa ili kuendelea kudumisha Amani, Uhuru, Udugu na Haki kwaajili ya ustawi wa nchi yetu.

Wiki hii ya Sheria inaongozwa na kauli mbiu ya miaka 100 ya Mahakama kuu nchini isemayo; “Mchango wa Mahakama katika nchi inayozingatia Uhuru, Haki, Udugu, Amani na Ustawi wa Wananchi 1921 – 2021”.

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waliokula Shilingi Milioni 932 za Halmashauri kufikishwa mahakamani.

    February 24, 2021
  • Wajumbe RCC waiomba Serikali kuhuisha Mradi wa VETA Sumbawanga ili kuwakomboa Wananchi.

    February 23, 2021
  • Shughuli za kibinadamu bado ni Changamoto katika uharibifu wa madaraja na barabara

    February 22, 2021
  • SITA WAFA KWA MATUKIO TOFAUTI IKIWEMO RADI

    February 18, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa