• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wanarukwa wahamasishwa kulima kwa tija ili kujiongezea kipato

imewekwa Tar: December 2nd, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wakulima wa Mkoa huo kuhakikisha wanafuata maelekezo ya maafisa kilimo waliopo kwenye ngazi za vijiji na kata ili kuweza kulima kwa tija na hatimae kuongeza upatikanaji wa chakula katika mkoa na pia kujiongezea kipato.

Amesema kuwa ni dhamira ya mkoa kuhamasisha kilimo kinachoongeza uzalishaji kwa ekari moja, hivyo ni lazima wakulima wapande kwa kutumia utaalamu huku wakizingatia ubora wa mbegu ambazo zimehakikiwa na Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu nchini (TOSC) pamoja na kutumia mbolea zinazostahili kwa ekari kama ambavyo wataalamu wanashauri

“Sio mtu anachukua mfuko mmoja wa mbolea halafu anakwenda kuuweka katika ekari mbili matokeo yake uzalishaji  unakuwa ni mdogo, lakini pia baada ya mahindi kuwa yameota na kuwekewa mbolea ni lazima pia kuangalia upande wa visumbufu, wadudu wale waharibifu wa mazao, lazima tuweke dawa mapema tutumie viuatilifu ambavyo vinashauriwa na wataalamu wa kilimo, baada ya hpo tuangalie mashamba yetu kwa kupalilia kwa kufanya hivi tunaweza kuzidfi hata gunia 20 kwa ekari,” Alisema.

Ameyasema hayo alipokuwa katika ziara yake maalum ya kuhamasisha kilimo chenye tija katika Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Mkoani humo akiwa pamoja na wataalamu wa kilimo wa mkoa na halmashauri pamoja na mkuu wa Wilaya hiyo.

Kwa upande wao mmoja wa wamiliki wa shamba lililotembelewa na Mkuu wa Mkoa Bwana Rojas Lukas amesema kuwa changamoto ubwa inayowakuta wakulima na kushindwa kuendelea kulima kilimo chenye tija ni mitaji pamoja na mdudu mharibifu aina ya kiwavi jeshi.

“Kuna mdudu Fulani anaitwa Kiwavi jeshi Yule anatusumbua sananingeomba serikali ijaribu kututafutia dawa ambayo inaweza ikamuua Yule mdudu, kingine tunaomba serikali itusaidie kama inawezekana watukopeshe ili tukuze kilimo chetu kiende mbele,” Alisema.

Akimkaribisha Mkuu wa mkoa katika shamba la mmoja wa wakulima hao mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Juliet Binyura alisema kuwa watalaamu wameendelea kutoa ushauri kwa wananchi mbalimbali na hivyo kuwaomba kuendelea kufanya hivyo ili kuwasaidia wakulima kuweza kufikia kilimo chenye tija.

“Tumekuja kuangalia utaalamu aliopewa kwa wataalamu ambao ni maafisa ugani katika kata yake na wanapanda kwa kutumia kamba na wanapima vipimo vinavyokubalika naamini ya kwamba mazao atavuna vizuri,” Alisema.

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waliokula Shilingi Milioni 932 za Halmashauri kufikishwa mahakamani.

    February 24, 2021
  • Wajumbe RCC waiomba Serikali kuhuisha Mradi wa VETA Sumbawanga ili kuwakomboa Wananchi.

    February 23, 2021
  • Shughuli za kibinadamu bado ni Changamoto katika uharibifu wa madaraja na barabara

    February 22, 2021
  • SITA WAFA KWA MATUKIO TOFAUTI IKIWEMO RADI

    February 18, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa