• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

WAZIRI LUGOLA AAGIZA POLISI KUWASAKA WABAKAJI WALIOKIMBILIA NCHINI ZAMBIA

imewekwa Tar: October 2nd, 2019

Na Felix Mwagara, MOHA, Rukwa.

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ametoa siku saba kwa Jeshi la Polisi Mkoani Rukwa, kuwasaka na kuwatia mbaroni wabakaji wanne waliokimbilia nchini Zambia. 

Lugola alisema wabakaji hao lazima wakamatwe na waletwe nchini kwasababu Jeshi hilo lina mbinu zote za kuwasaka wahalifu hao wanaodaiwa kukimbia kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa baada ya kubainika kufanya uhalifu huo Wilayani Kalambo.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Mji wa Matai wilayani Kalambo Mkoani humo, Lugola alisema Wilaya hiyo inakabiliwa na matukio mengi ya ubakaji ambapo mpaka sasa Polisi tayari imewatia mbaroni wabakaji 11 na bado hao wanne wanaendelee kutafutwa ili wakamatwe.

Lugola alisema kero alizopewa na wananchi hao katika mkutano wa hadhara zikiwemo ubakaji kuwa juu pamoja na idadi kubwa ya wanafunzi kuachishwa masomo kwa ajili ya kufanyishwa kazi wakiwa na umri mdogo, pamoja na wanafunzi kubakwa na kupewa mimba. 

“Haiwezekani wahalifu waichezee Serikali ya Rais Dkt. Magufuli, lazima wakamatwe, wasakwe kwa nguvu zote, na mnipe taarifa mtakapowatia mbaroni watuhumiwa hao,” alisema Lugola. 

Aliongeza kuwa, wahalifu mbalimbali wakiwemo majambazi, kutokana na uimara wa Jeshi la Polisi wamesambaratishwa na wanaendelea kusakwa katika kona zote nchini mpaka jambazi wa mwisho atakapotiwa mbaroni.

Aidha, Lugola aliwataka wananchi kutoa taarifa kwake na kwa viongozi wa Polisi wa Wilaya na Mkoa endapo kuna mwananchi atabambikiziwa kesi au kuombwa rushwa wakati anamuombea dhamana ndugu yake.

Lugola alikiri kuwepo kwa baadhi ya polisi wanaoendelea kuwaomba rushwa wananchi ili wapate dhamana pamoja na kubambikiwa kesi

   “Ndugu wananchi, hili nilishaliagiza na pia naendelea kuliagiza, ni marufuku kwa askari polisi yeyote atakaye muomba rushwa mwananchi ili ndugu yake apewe dhamana, dhamana ni haki ya mwananchi, na uikiingia polisi bure na kutoka ni bure,” alisema Lugola.    

Pia Waziri Lugola alisisitiza kuwa, dhamana zitolewe saa 24 nchini bila wananchi kuombwa rushwa ya aina yoyote, na kuonya kuwa askari atakayepuuza agizo hilo, ataondolewa ndani ya Jeshi la Polisi. 

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kalambo, Deokresi Mkandala alipokea maagizo ya Waziri Lugola likiwemo la kuwasaka wahalifu hao waliokimbilia nchini Zambia na kuahidi kuyafanyia kazi.

Waziri Lugola anaendelea na ziara yake Mkoani Rukwa kutatua kero mbalimbali za wananchi kupitia mikutano ya hadhara katika Wilaya zote mkoani humo.

  








Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Waomba Daraja la muda baada ya watu wanne kuzama mtoni

    February 27, 2021
  • Wananchi walazimika kuzunguka Zaidi ya Km 30 kufuata huduma kwa kukosa barabara ya km 7.3.

    February 26, 2021
  • Helium Yaibuka Kikao cha Bodi ya Barabara na kuibua gumzo.

    February 25, 2021
  • Waliokula Shilingi Milioni 932 za Halmashauri kufikishwa mahakamani.

    February 24, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa