Tarehe 31/08/2018 VETA Makao Makuu Dar es Salaam, VETA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Mbeya pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa tulifanya hafla fupi ya kumkabidhi Mkandarasi TENDER INTERNATIONAL kiwanja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi (VETA) katika Manispaa ya Sumbawanga pamoja na Mkandarasi, Mshauri Elekezi (Consultant) Sky Architect Consultancy Ltd.
Eneo hilo ambalo VETA itajengwa lipo Kashai (MUVA) katika Manispaa ya Sumbawanga na lina ukubwa wa 95,934 sq M Plot 1 Block ‘A’ (LD) chenye hati Namba 44102-MBYLR iliyotolewa tarehe 5 Machi, 2018.
Mradi unategemewa kukamilika ndani ya miezi 12 (kuanzia tarehe ya makabidhiano). Aidha, gharama za ujenzi za mradi huu ni Tsh. 10,700,488,940.05. Ujenzi ukikamilika chuo kitaweza kuchukua wanafunzi 900 wa kozi ndefu na 600 wa kozi fupi hivyo, kitakuwa na uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 1,500.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani
Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA
Simu: 025 280 2137
Simu: 0735019734
barua pepe: ras@rukwa.go.tz
Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa