• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kilimo

Kilimo cha zao la kahawa

Mkoa unaendelea na juhudi za kufufua zao la kahawa kwa kuweka msukumo katika usimamizi ili zao hili liweze kuwa moja ya zao la biashara katika Mkoa wetu. Juhudi hizi ni pamoja na kuhamasisha wakulima, kutambua maeneo ya kilimo, kuwapatia mafunzo wakulima na wataalam na kuzalisha miche.

Eneo litakalolimwa zao la kahawa

Baada ya kuhamasisha wakulima, makampuni na taasisi, eneo la kiasi cha ekari 3,195.83 kimebainika kuwa kitafaa kulimwa zao la kahawa. Jumla ya wakulima 2,266 na taasisi 9 zitajihusisha katika uzalishaji wa kahawa.

 

Kazi zilizofanyika

Ili kuhakikisha juhudi za kufufua zao hili zinafanikiwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ilizielekeza Halmashauri kwenye kikao cha tarehe 10 Januari, 2018 kuanza jitihada za kufufua na jitihadi zilizofanyika ni kama ifuatavyo;

  • Kuwasilisha taarifa ya nia ya kulima zao la kahawa katika  vikao vya mbalimbali vya Halmashauri.
  • Kuandaa daftari la wakulima wa zao la kahawa.
  • Kutenga bajeti kiasi cha shilingi 79,000,000 katika mwaka 2018/2019 kwa ajili ya zao hili.
  • Kuwezesha mafunzo ya kujenga uelewa kwa wakulima 20 na mafunzo ya kujenga uwezo kwa wataalam 19 katika  kituo cha Utafiti cha TaCRI Mbimba.
  • Kuanzisha vitalu kwa ajili ya kuzalisha miche.

 

Kilimo cha zao la alizeti.

Mkoa umejipanga katika kuhamasisha kilimo cha zao la alizeti kama zao la biashara. Hali ya uzalishaji wa zao la alizeti katika mkoa umebaki kuwa ni wastani wa gunia  6.5 za kilo 65  kwa ekari sawa na  tani 1.1 kwa hekta. Tija hii ni ndogo sana ukilinganisha na tija iliyofanyiwa utafiti ya gunia 12-16 kwa ekari sawa na Zaidi ya tani 2.00 kwa hekta

Sababu za kuwa na uzalisha mdogo ni pamoja na :-

  • Matumizi ya mbegu ambazo hazizalishwa kitalaam,
  • Uchache wa mbegu bora za zao la alizeti,
  • Kutotumia mbolea na viutilifu,
  • Bei kubwa ya mbegu  chotara (hybrid) zenye tija kubwa, 
  •  Kutolipa umuhimu unaostahili zao la alizeti kama ilivyo kwa zao la mahindi katika mkoa.

Mkakati wa mkoa  ni kufikia malengo yafuatavyo:-

  • Kuongeza tija ya zao la alizeti kutoka 1.1 tani/hekta hadi 2.0 tani/hekta ifikapo  mwaka 2020/2021
  • Kuongeza eneo linalolimwa alizeti kutoka hekta 47,862.1 hadi hekta 200, 000 ifikapo mwaka 2020/2021.
  • Kuongeza uzalishaji wa alizeti kutoka tani 53,470.5 hadi tani 400,000 kwa mwaka ifikapo mwaka 2020/2021.
  •  Kuongeza ubora wa mafuta, vifungashio na uwezo wa wasindikaji wa mafuta katika mkoa.
  •  Kuongeza matumizi ya mbegu bora (chotara) za alizeti kwa asilimia 50% ifikapo mwaka 2020/2021
  • Kuongeza idadi ya viwanda vikubwa vya kusindika alizeti kutoka 0 hadi 3 ifikapo  mwaka 2020/2021

 

Mkakati wa kufikia malengo.

  • Mkakati huu utatekelezwa kwa kuwahusisha wadau mbalimbali waliopo katika Mkoa. Wadau hao ni pamoja na mkulima mmoja mmoja, vikundi vya wakulima, Halmashauri, wasindikaji, makampuni ya pembejeo n.k.
  • Kupitia jukwaa la alizeti la mkoa kutakuwa na majadiliano ya kina juu ya uendelezaji wa zao la alizeti katika mkoa. Jukwaa hili litawahusisha wakulima, wasindikaji, wasambazaji wa pembejeo na wadau wengine.
  • Mkakati unawatambua wadau mbalimbali wa alizeti watakaosaidiana na serikali katika kuendeleza zao hili. Wadau hao ni pamoja na SNV, vituo vya utafiti, AMDT, FAIDA MALI na makampuni mbalimbali.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa