• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Elimu

Seksheni hii ina lengo la kusaidia au kuwezesha utoaji huduma za uendelezaji wa Elimu ikijumuisha usimamizi wa elimu ya awali, msingi, sekondari, elimu ya watu wazima na inayotolewa katika njia isiyo rasmi; na mitihani ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu. Seksheni hii inaongozwa na Katibu Tawala Msaidizi ambaye pia ni Afisa Elimu wa Mkoa ambaye anawajibika kwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Majukumu ya Seksheni ya Huduma za Elimu

  1. Kuratibu uongozi wa shule za awali, Msingi, Sekondari, elimu ya watu wazima na Elimu rasmi
  2. Kuratibu ajira na usambazaji wa walimu wa shule za awali, msingi na sekondari katika Mkoa
  3. Kuratibu utekelezaji wa sera za Elimu na mafunzo ya ufundi ndani ya Mkoa na kutoa Ushauri kadiri inavyohitajika.
  4. Kusimamia mitihani ya shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu katika Mkoa.
  5. Kuratibu ukusanyaji, tathimini, uunganishaji/uandaaji, kutafsiri na kutoa taarifa/takwimu za elimu na mafunzo ya ufundi katika Mkoa
  6. Kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa taarifa za ukaguzi
  7. Kuzishauri Mamlaka za Serikali za Mitaa juu ya utekelezaji wa sera ya utamaduni na michezo
  8. Kuratibu shughuli zinazohusiana na michezo katika Mkoa na kuendesha mashindano ya UMITASHUMTA na UMISETA Mkoani.

ELIMU YA AWALI

Idadi ya Shule zenye madarasa ya Elimu ya Awali ni 367 (Serikali 358 na zisizo za Serikali 9). Shule ya msingi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum ya Malangali katika Manispaa ya Sumbawanga ndio inayokosa darasa la Elimu ya Awali.

Idadi ya wanafunzi Elimu ya Awali waliotarajiwa kuandikishwa ni 37,622 (wavulana 18,642 wasichana 18,980). Idadi ya walioandikishwa ni 43,065 (wavulana 21,108 wasichana 21,957) sawa na asilimia 112.  Hivyo kuna ongezeko la wanafunzi 5,443.

ELIMU YA MSINGI

Idadi ya Shule za msingi ni 368 (Serikali 359 na zisizo za serikali 9).

Idadi ya wanafunzi waliotarajiwa kuandikishwa darasa la kwanza ni 49,518 (wavulana 24,587 wasichana 24,931). Idadi ya walioandikishwa ni 71,582 (wavulana 35,323 na wasichana 36,259) sawa na asilimia 144.  Kuna ongezeko la wanafunzi 22,064.

Idadi ya wanafunzi katika shule za msingi darasa la I-VII ni 252,355 (Wavulana ni 123,537 wasichana 128,818).

Mahitaji ya walimu ni 6508 wakati waliopo ni 4189 na upungufu  ni 2319 sawa na 36%.

ELIMU YA SEKONDARI

Mkoa wa Rukwa una idadi ya shule za Sekondari zipatazo 90 kati ya hizo shule za Serikali zikiwa 69 na zisizo za serikali 21. Kati ya shule 90 za Sekondari zilizopo Shule 13 zina kidato cha 5 na 6 (Serikali 10 na zisizo za Serikali 3). Aidha shule 3 za Serikali zimepata Kidato cha 5 kwa mwaka 2017 ambazo ni; Kipeta, Mpui na Vuma zilizoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga.  Shule hizi zimepangiwa wanafunzi wa kidato cha tano kama ifuatavyo; Kipeta wavulana 36, Vuma wavulana 68 na Mpui wasichana 36.

Idadi ya wanafunzi kwa shule za Sekondari za Serikali ni 27939 (wav 14,942 na was 12,997)

Mahitaji ya walimu ni 1724, waliopo ni 1511 upungufu ukiwa walimu 213.  Upungufu huu ni kwa walimu wa Sayansi tu. Aidha, Mkoa ulipangiwa walimu wapya 91 wa masomo ya Sayansi, Hisabati na Wataalam wa Maabara 10. Walioripoti ni walimu 80 na Wataalam wa Maabara 6.

ELIMU MAALUMU

Mkoa una shule moja ya Elimu Maalumu ambayo ni shule ya msingi Malangali iliyopo Manispaa ya Sumbawanga.  Aidha kuna Vitengo 14 kama inavyojionesha kwenye jedwali 

Halmashauri

S/n

Kitengo

Aina ya Ulemavu

Idadi ya wanafunzi

Wav

Was

Jml

Kalambo

1

Mbuluma
Viziwi

3

0

3

Mtindio wa Ubongo

1

1

2

Viungo

1

0

1

2

Kilesha
Mtindio wa ubongo

3

2

5

Uoni hafifu

2

2

4

3

Kipwa
Mtindio wa ubongo

5

3

8

Bubu

2

0

2

Viungo

3

2

5

4

Myunga
Mtindio wa ubongo

5

2

7

Uoni hafifu

3

1

4

Viungo

3

2

5

Viziwi

2

0

2

5

Matai ‘A’
Bubu

2

1

3

Mtindio wa ubongo

2

2

4

Usonji

0

1

1

Viungo

0

1

1

6

Msanzi ‘A’
Mtindio wa ubongo

3

2

5

Bubu

0

1

1

Viungo

1

0

1

Nkasi

7

Isunta
Ulemavu wa akili

14

8

22

Viziwi

3

1

4

8

Machete
Ulemavu wa akili

6

4

10

9

Kirando
Ulemavu wa akili

3

6

9

Viziwi

2

1

3

Uoni hafifu

0

1

1

Ulemavu wa viungo

3

2

5

Sumbawnga (M)

10

kizwite
Viziwi

17

11

28

Ulemavu wa akili

11

3

14

Ulemavu wa ngozi

21

21

42

Uoni hafifu

10

12

22

Wasioona

10

17

27

11

Katandala
Ulemavu wa akili

4

3

7

12

Mwenge
Ulemavu wa akili

5

8

13

Sumbawanga (V)

13

Laela ‘A’
Ulemavu wa akili

6

4

10

14

Mukamanye
Ulemavu wa akili

2

2

4

Viziwi

1

3

4

JUMLA

159

130

289


ELIMU YA UALIMU:

 Mkoa una jumla ya Vyuo vya Ualimu vinne (4) ambapo Vyuo vitatu (3) vinamilikiwa na Taasisi zisizo za Serikali ambavyo ni; Chuo cha Ualimu Aggrey, Rukwa na St. Maurus na Chuo kimoja (1) cha Ualimu cha Serikali ambacho ni Sumbawanga.

VYUO VYA UFUNDI STADI

Mkoa unavyo Vyuo vya Ufundi Stadi vipatavyo 4, kama inavyooneshwa katika jedwali.


    • NA
    • HALMASHAURI
    • VYUO VYA UFUNDI STADI
    • SERIKALI
    • BINAFSI

    • Kalambo
    • Mwazye shule ya Msingi
    • -
    • Matai shule ya Msingi
    2.
    • Nkasi
    • -
    • Mvimwa shule ya Msingi
    3.
    • Sumbawanga (M)
    • Katandala “B” shule ya Msingi
    • Furaha Center


ELIMU YA CHUO KIKUU

Mkoa una kituo 1 cha chuo kikuu Huria na Chuo kikuu cha Sayansi Tawi la Mbeya (Mbeya Universty of Sience and Technology- MUST) kilichopo katika eneo lililokuwa kambi ya ujenzi la Kianda katika Halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga. Hadi sasa Chuo kikuu cha MUST kimeshakabidhiwa eneo hilo pamoja na majengo yaliyokuwa kwenye kambi hilo kwa ajili ya kuanza kazi

Matangazo

  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • JAMII ISHIRIKIANE NA WALIMU KUKUZA TAALUMA

    February 16, 2023
  • Kampeni Upandaji Miti

    February 07, 2023
  • TASAF

    February 05, 2023
  • RAS Mchatta akagua miradi

    January 26, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa