• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Viwanda

Sekta ya Viwanda na biashara ni muhimu sana katika Mkoa wetu kwani inasaidia katika kuongeza ajira kwa wananchi na kukuza uchumi wa Mkoa na nchi kwa ujumla. Katika sekta hii kuna viwanda vidogo na vya kati vinavyoendeshwa. Viwanda hivyo vinahusisha shughuli za usindikaji wa nafaka, samaki, nyama na kiwanda cha kutengeneza sabuni.

Kwa upande wa biashara, Mkoa umekuwa ukijitahidi katika kuhakikisha kuwa inawakwamua wananchi wake kiuchumi. Katika jitihada hizo maafisa biashara wamekuwa wakitoa elimu na ushauri kwa wajasiriamali juu ya kuendesha biashara zao kwa mafanikio na uboreshaji wa vifungashio kwa wasindikaji ili kuwavutia wateja na

kuongeza mauzo. Pia wamekuwa wakitoa elimu juu ya umuhimu wa ulipaji wa kodi kwa wakati na kuwapa na leseni za biashara.

Sekta ya Viwanda na biashara ni muhimu katika  kuongeza ajira kwa wananchi na kukuza uchumi wa Mkoa. Viwanda vilivyopo katika mkoa ni viwanda vidogo sana na vya kati vinavyoendeshwa na sekta binafsi. Viwanda hivyo vinashughulika na usindikaji wa nafaka, samaki, nyama na maji. Mkoa  una maeneo mengi yanayofaa kwa  uwekezaji  wa viwanda hasa katika maeneo yafuatayo:-

  1. Kilimo,
  2. Mifugo,
  3. Uvuvi ,
  4. Sekta ya Nishati na madini,

Jumla ya hekta 809. Zimeanishwa katika Halmashauri kwa ajili ya kuvutia sekta binafsi kujenga viwanda vya aina mbalimbali

Idadi ya viwanda vilivyopo katika mkoa 

Kwa mujibu wa orodha ya viwanda Tanzania Bara kwa takwimu za Desemba 2015 - Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Mkoa wa Rukwa una takribani viwanda 950 (viwanda vidogo sana 869,  ni viwanda vidogo 78,Viwanda vya kati 2 kiwanda kikubwa  1)

Jedwali Na. -------- idadi ya viwanda vilivyopo katika mkoa kwa kigezo cha ajira.

Aina ya kiwanda
Idadi ya waajiriwa
Idadi ya viwanda
Asilimia 
Viwanda vidogo sana
1 hadi 4

869

91.50

Viwanda vidogo)
5 hadi 49

78

8.2

Viwanda vya kati
50 hadi 99

2

0.2

Viwanda vikubwa
100 na zaidi

1

0.1

JUMLA 

950

100.00

Mikakati wa mkoa wa kuendeleza viwanda.

  1. Utekelezaji wa ujenzi wa viwanda nchini kwa kiwango kikubwa utategemea ushiriki wa sekta binafsi. Ili kufanikiwa katika Mkakati wa kuendeleza na kujenga viwanda katika Mkoa mambo yafuatayo yanatakiwa kuzingatiwa na wadau wote:-
  2. Upatikanaji wa Ardhi kwa ajili ya uwekezaji wa Viwanda na Masoko.
  3. Kuimarisha na kuendeleza miundombinu ya SIDO.
  4. Upatikana wa maeneo ya kujenga Ofisi na maeneo ya viwanda kwa ajili ya SIDO katika Wilaya.
  5. Kuwezesha upatikanaji wa teknolojia rahisi na nafuu hususan kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza Viwanda Vidogo na vya Kati kwa ajili ya kuchochea uanzishaji wa viwanda vikubwa
  6. Kuhamasisha ushiriki wa Sekta Binafsi kupitia elimu na mafunzo ya kuendesha na kuendeleza viwanda, ujasiriamali na uwekezaji kwa kushirikiana  au kushirikisha wadau mbalimbali vikiwemo vyombo vya habari, taasisi za elimu, vyama vya wazalishaji, wasambazaji na walaji wa bidhaa za viwanda
  7. Kuanzisha vituo vya maonesho ya bidhaa za wajasiriamali, viwanda vidogo na kuwa na ratiba endelevu za maonesho hayo na kuwezesha wadau hawa kushiriki katika soko la ndani na la kimataifa kupitia maonesho ya biashara.
  8. Kuwaunganisha wajasiriamali na taasisi za fedha zinazotoa mikopo nafuu ikiwa ni pamoja na Mfuko wa Taifa wa Maendeleo ya Wajasiriamali (NEDF) unaotoa mikopo midogo kwa wenye viwanda na wafanyabiashara wadogo.
  9. Kuendelea kuboresha miundombinu ya msingi na kuifikisha katika maeneo na shughuli za wawekezaji ili kuwezesha maendeleo ya viwanda hususan, upatikanaji wa uhakika wa nishati ya umeme na maji, ujenzi wa barabara, uwanja wa ndege na bandari
  10. Kushirikisha wananchi na wadau katika hatua mbalimbali za hifadhi na utunzaji wa mazingira na kujenga uwezo wa kitaasisi katika kuimarisha mifumo itakayosaidia kuhimili mabadiliko ya tabia nchi.
  11. Kusimamia utekelezaji wa sheria na taratibu na kuhakikisha kuwepo kwa utulivu, amani na usalama wa ndani ya mkoa na taifa kwa ujumla.
  12. Kuanzisha kongano za viwanda ( Industrial Clusters ) za kuongeza thamani ya mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi na misitu katika kila Halmashauri.
  13. Kuhamasisha umoja na ushirika wafugaji ili kwa pamoja waweze  kuwa na maeneo ya ukusanyaji maziwa na viwanda vya kusindika mazao ya maziwa

Agenda ya Viwanda 100 kila Mkoa - 30 Juni, 2019

Katika kutekeleza Agenda ya uanzishwaji wa viwanda 100 Mkoa  umefanikiwa kujenga viwanda vipya 124 kati ya hivyo vidogo sana ni 86, vidogo 36, cha kati 1 na kikubwa 1.

Hadi kufikia 30 Juni, 2019 Mkoa wetu ulikuwa na jumla ya viwanda 1,024 kwa mchanganuo ufuatao:-

Viwanda vikubwa 5,

Viwanda vya kati 4,

Viwanda vidogo 120, na

Viwanda vidogo sana 895

Jedwali Na: 8 Mchanganuo wa viwanda vilivyopo katika Mkoa

Na.
Ukubwa wa kiwanda
Aina ya kiwanda
Idadi
1
Vidogo sana
Usindikaji nafaka(mahindi)
644
2
Ushonaji nguo
228
3
Ushonaji viatu
4
4
Utengenezaji majiko ya kupikia
11
5
Uhunzi
8

Jumla ya Viwanda vidogo sana

895
6
Vidogo
Usindikaji nafaka(mahindi)
29
7
Kusindika nafaka(mpunga)
24
8
Ukamuaji Alizeti
19
9
Utengenezaji wa samani
12
10
Uokaji mikate na maandazi
5
11
Usindikaji wa Samaki
5
12
Utengenezaji wa sabuni
1
13
Uchomeleaji
25

Jumla ya Viwanda vidogo

120
14
Vyakati
Usindikaji nafaka (mahindi)
3
15
Kiwanda cha Gesi
1

Jumla ya Viwanda vya Kati

4
16
Vikubwa
Usindikaji nyama
1
17
Uzalishaji wa Makaa ya mawe
1
18
Usindikaji nafaka(mahindi)
2
19
Uzalishaji wa maji
1

Jumla ya Viwanda vikubwa

5
Jumla kuu ya Viwanda Kimkoa
1,024

Baadhi ya Bidhaa za Viwanda zinazopatikana katika  katika Mkoa

Kiwanda cha Maji ya kunywa cha Dew Drop

 

Kiwanda cha Energy Milling, Sumbawanga.

SAAFI kiwanda cha Nyama

Mahindi yanapatikana kwa wingi Rukwa

Mpunga ni miongoni mwa Zao Kuu la Kibiashara katika Mkoa wa Rukwa



Viazi Lishe navyo hurahisishwa na kuwa chakula kitamu


Samaki wa Kukaushwa wa Ziwa Rukwa  


Asali pia inapatikana kwa Wingi katika Wilaya zote za mkoa wa Rukwa


Mafuta ya Karanga yanapatikana Sumbawanga


Unga wa Mahindi ya njano


Ulezi, Ngano na Unga wa ngano.


Dagaa Kutoka Ziwa Tanganyika, Wilaya za Nkasi na Kalambo


Unga wa Muhogo wa Wilaya ya Nkasi


Samaki aina ya Mikebuka


Mchele safi wa Rukwa 


Maharage aina ya Ulambo


Unga wa Dona


Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa