• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Miundombinu ya Rukwa

Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga 

Serikali kupitia mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania imepata mkopo nafuu kiasi cha Shilingi Billion 55.9 kutoka Benki ya Maendeleo ya Ulaya (EUROPEAN INVESTMENT BANK – EIB) kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja hiki kwa kiwango cha kimataifa. Na Serikali italipa kiasi cha Tanzania Shilingi Billion 3.3 kwa Wahanga wapatao 97, kutoka Kata zote mbili yaani Kata ya Sumbawanga Asilia wapato 27 na Kata ya Izia 70 na kufikia jumla ya Wahanga 97. Kazi hii itahusisha (Scope) maeneop yafuatayo;

  • Ujenzi wa Jengo jipya la Abiria na miundombinu yake.
  • Ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege kwa kiwango cha lami (Paved Runway).
  • Barabara ya kiungio kutoka kiwanjani na maegesho ya magari kwa kiwango cha lami.
  • Usimikaji wa mfumo wa taa pamoja na mitambo ya kuongozea ndege (AGL & NAVAAIDS).

Baada ya ujenzi huu kukamilika utawezesha kiwanja cha ndege cha Sumbawanga kutumika kwa masaa 24 na kipindi chote cha mwaka.

Ziara ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi Mh. Atashasta Nditiye walipopita katikati ya Uwanja wa Ndege wa Sumbawanga

Mpango wa Kujenga Kiwanja cha Ndege Eneo la Kisumba

Mkoa umetenga eneo lenye ukubwa wa Hekari 3,411 katika eneo la Kisumba Manispaa ya Sumbawanga kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege. Eneo hili linamilikiwa na Meneja, Kiwanja cha Ndege Sumbawanga. Matarajio ni kujenga Kiwanja cha Ndege cha kisasa ili kuongeza fursa za usafiri na kuchochea shughuli za kiuchumi. Kwa mujibu wa Meneja wa TANROADS ambaye ana dhamana ya ujenzi na ukarabati wa Viwanja vya Ndege, usanifu (Design) unatarajiwa kuanza Mwaka wa Fedha 2019/2020

Uboreshaji wa bandari zilizopo katika Mkoa wa Rukwa

Bandari ya Kasanga

Bandari ya Kasanga ina Gati la kuegesha Meli lenye urefu wa Mita 20 na kina cha maji cha mita 8-10 kutegemeana na msimu wa mvua pia lina uwezo wa kuhudumia meli moja kwa wakati mmoja. Katika kipindi cha miaka mitatu 2014/2015 – 2016/2017, bandari ilihudumia jumla ya tani 63,310 kati ya hizo tani 57,739 ilikuwa ni shehena ya kwenda nje ya Nchi (Export) na tani 5,571 ilikuwa ni shehena ya kwenda ndani ya Nchi (Inward/ Outward).

Upanuzi wa Bandari ya Kabwe

Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imeanza kufanya upanuzi wa Bandari  ya Kabwe. Upanuzi  huo unatarajia kugharimu Shilingi bilioni 7.5. Aidha, Mkandarasi SUMRY ENTERPRISES LTD ameingia Mkataba wa kufanya kazi hiyo kwa muda wa miezi 18 kuanzia tarehe 2 Aprili, 2018. Mamlaka ya Bandari tayari imekwisha lipa fidia kiasi cha Shillingi 160,743,498.00 kwa wananchi  37 waliopisha eneo hilo kwa ajili ya  ujenzi wa miundombinu ya bandari.

Bandari ya Kipili 

Novemba, 2015 – Juni, 2016 Bandari ilipokea shehena ya Tani 1298, Julai, 2016 – Juni, 2017 Bandari ilipokea shehena ya Tani 978, Julai 2017 – Juni, 2018 Bandari ilipokea tani 626. Maeneo yafuatayo yanatakiwa kuboreshwa ili kuongeza ufanisi;

  • Barabara ya kwenda bandarini
  •  Umeme kufikishwa bandarini toka kijiji cha Kipili
  • Kuhamasisha Wadau mbalimbali kutumia bandari, ikiwa ni pamoja na Wafanyabiashara kutoka DRC.

 Mawasiliano ya Kidigitali

Mkongo wa Taifa (NICTBB)

Mkoa wa Rukwa unahudumia jumla ya vituo vitatu (3) vya mkongo wa Taifa ambavyo ni Miangalua, Sumbawanga T/House na Kizi.. Aidha Mkoa unahudumia jumla ya km 240 ya mkongo wa Taifa zilizogawanyika kama ifuatavyo:

  • Miangalua -Sumbawanga (119km),
  • Sumbawanga- Kizi (121km),

Wateja wa Mkongo wa Taifa

TTCL inaendelea kuhakikisha kuwa inakuwa ndio muhimili wa teknolojia ya habari na Mawasiliano (Tehama) nchini; na  leo TTCL kwa Mkoa wa Rukwa na Katavi imeunganisha wateja mbali mbali kwenye mkongo wa Taifa kama ifuatavyo:-

SUMBAWANGA: TANROAD, TRA, TANESCO, Mahakama ya Mkoa, Benki ya Posta, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Hazina ndogo, Sumatra, Water Reed, Manispaa ya Sumbawanga, Halmashauri ya Sumbawanga, NSSF, NHIF, NMB, CRBD, TPC, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Hospitali ya Rufaa Rukwa, NIC, SUWASA , MUST RUKWA Campus, Chuo Kikuu Huria na Maktaba ya Mkoa.

Shirika la Posta Tanzania 

Utekelezaji wa kazi zinazofanywa na Shirika la Posta

 Ofisi kuu ya Shirika la Posta Mkoa wa Rukwa ipo barabara kuu mtaa wa Mbeya Road, mkabala na Hospital kuu ya Mkoa wa Rukwa, Sumbawanga.

Huduma zinazotolewa na Shirika la Posta Rukwa 

  • Huduma za barua
  • Huduma ya utumaji na ulipaji wa fedha kwa njia ya mtandao
  • Huduma ya Expedited Mail Services (EMS)
  • Huduma ya Advertising Mails., matangazo kupitia masanduku ya barua
  • Huduma ya Internet Café na photocopy
  • Huduma za uwakala (Benki ya Posta,CRDB,NSSF,Moneygram, na Western Union)
  • Huduma ya Pcum, ukusanyaji sampuli za damu kavu (dried Blood Spot) kwenye vituo vya afya.
  • PostGiro, kupokea na kufanya malipo kwa niaba ya mteja

Ujenzi wa barabara 

Sumbawanga - Matai kasanga port (km 112)

Kazi ya ujenzi wa barabara bado inaendelea. kwa ujumla kazi imekamilika kwa asilimia 71.6 na kutarajiwa kumalizika 30 Septemba 2018. 

Miundombinu ya Barabara 

Mkoa wa Rukwa una barabara zenye urefu wa kilometa 1,245.60 zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambazo zinasimamiwa na Ofisi ya Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Rukwa. Kati ya barabara hizo, kilometa 407.94 ni Barabara Kuu (Trunk Roads) na kilometa 837.66 ni Barabara za Mkoa (Regional Roads). Mchanganuo wa aina na urefu wa barabara hizo ni kama inavyoonyeshwa katika Jedwali Na.10 hapa chini.

Kwa upande wa Miundombinu, Serikali imeendelea kujenga na kukarabati barabara pamoja na Miundombinu mingine.  Barabara mpya zilizoanza kujengwa katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nne zimekamilika.  Barabara hizo ni zifuatazo:-

  • Sumbawanga  - Chala – Kanazi (Km 75)
  • Kanazi  -Kizi  - Kibaoni (Km 76.6)
  • Sumbawanga  - Matai  - Kasanga Port (Km. 112) (Ujenzi umefikia asilimia 91)

Na

Jina la Mradi

Aina ya Mradi

Gharama (Sh. Milioni)

Muda wa Utekelezaji (Tarehe)

Maendeleo na Maelezo Mengine Muhimu

Kuanza

Kwisha

1
Sumbawanga – Chala - Kanazi
Ujenzi kwa kiwango cha lami

78,840.600

10.3.2013
31.11.2017
Kazi imekamilka
2
Kanazi – Kizi - Kibaoni
Ujenzi kwa kiwango cha lami

82,841.779

10.4.2010
31.7.2017
Kazi imekamilika
3
Sumbawanga – Matai – Kasanga Port
Ujenzi kwa kiwango cha lami

133,286.603

13.1.2010
11.11.2018
Kazi inaendelea
4
Matai - Kasesya
Ujenzi kwa kiwango cha lami

 



Kazi bado kutangazwa
5
Momba Bridge
Ujenzi wa daraja la Momba

17,718.145

24.7.2014
24.7.2019
Kazi imekamilika
6
Sumbawanga Airport
Ujenzi  kiwango cha lami

55,908.850



Fidia imelipwa. Ujenzi bado kuanza


TARURA

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tanzania Rural and Urban Roads Agency) kwa kifupi TARURA umeanzishwa rasmi kwa mujibu wa Sheria ya Wakala za Serikali Sura 245 (Executive Agencies CAP 245) na kutangazwa rasmi katika Gazeti la Serikali Na. 211 la tarehe 12/05/2017.

Wakala huu umeanzishwa rasmi tarehe 1/7/2017 kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya kiutendaji zaidi kuhusu maendeleo ya barabara za vijijini na mijini. Majukumu hayo ni ya ujenzi, matengenezo pamoja na menejimenti ya barabara za vijijini na mijini.

Mtandao wa Barabara za Mkoa wa Rukwa

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini kwa Mkoa wa Rukwa unasimamia matengenezo ya barabara zenye urefu wa Km 2,304.18, kati ya lami/zege ni km 34.22,changarawe km 694.09, udongo Kilomita 1,575.87 na vivuko 1,986 vya aina tofauti kama ilivyofafanuliwa hapa chini kwenye Jedwali  Na.12 Takwimu hizo ni hadi mwezi Juni, 2019.


Daraja kubwa lenye urefu wa mita 84 Mto Momba

Ujenzi wa daraja la Momba katika eneo la Kilyamatundu/Kamsamba lenye urefu wa meta 84 imekamilka. Kazi ya ujenzi wa daraja inafanywa na Mkandarasi Jiangxi Geo-Engineering (Group) Corporation kutoka China kwa gharama ya Shilingi million 17,718.145. Mkataba wa ujenzi ulisainiwa tarehe 14 Julai, 2017 na kazi ilianza tarehe 1 Agosti, 2017. Kazi ya ujenzi itachukua muda wa miezi kumi na tatu (13) kukamilika ikijumuisha mwezi mmoja wa maandalizi. Kazi ya ujenzi wa daraja ilitarajia kukamilika ifikapo tarehe 31 Agosti 2018. Hata hivyo kazi haikuweza kukamilika kutokana na mto kujaa maji nakupelekea kuongenza muda wa kukamilisha kazi hadi tarehe 24 Julai, 2019. Kazi ya ujenzi imekamilika na daraja linapitika.

Kazi ya Usimamizi inafanywa na TANROADS Engineering Consultancy Unit (TECU) chini ya Meneja wa TANROADS Mkoa wa Rukwa. Gharama ya usimamizi hadi sasa ni Shilingi milioni 353.80625. 


Huduma za Kibenki 




Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa