• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Minerals

SEKTA YA MADINI

Umuhimu na Nafasi ya Sekta ya Madini Katika Mkoa.

Kama ilivyoelekezwa katika ibara ya  64 ya ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 - 2025 kuwa serikali ya Mkoa itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wanaohitaji kuwekeza katika madini.

Mkoa umebarikiwa kuwa na rasilimali ya madini mbalimbali. Hata hivyo kwa sasa kuna leseni mbili tu za uchimbaji wa kati (Mining Licence) hivyo kupelekea uchimbaji wa madini haya kuwa ni kwa kiasi kidogo na kufanywa na wachimbaji wadogo (Small Scale Miners). Mkoa unatambua umuhimu na nafasi ya madini katika kuchangia pato la taifa na la mwananchi mmoja mmoja. Kwa kulifahamu hilo, mkoa unaweka mazingia mazuri ya upatikanaji wa umeme, uboreshaji wa miundombinu ya barabara na mawasiliano ili kuvutia wawekezaji kuja kuwekeza katika uchimbaji wa madini mbalimbali ndani ya mkoa.

Fursa za uwepo wa madini mbalimbali zimetangazwa kwenye makongamano mbalimbali yaliyofanyika ndani na nje ya Mkoa (Mwaka 2007), Kanda ya Magharibi ya Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma (Miaka ya 2012, 2013 na 2014) na Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Rukwa (Mei, 2023). Aidha, maelezo hayo yanapatikana kwenye tovuti ya Mkoa na Halmashauri.

Ofisi ya Madini Mkoa

Katika Mwaka wa Fedha 2018/19, Tume ya Madini ilifungua Ofisi ya Madini Mkoa wa Rukwa (RMO – Rukwa). Ofisi hii imeanza kazi tarehe 09/11/2018 na inasimamia shughuli zote za madini katika Wilaya zote za Mkoa wa Rukwa na Halmashauri zake (Nkasi, Kalambo, Sumbawanga Manispaa na Sumbawanga Vijijini).

Soko la Madini

Ofisi ya Madini Mkoa wa Rukwa kwa kushirikiana Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa tayari imefungua Soko la Madini ambalo lipo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Hata hivyo, kuna mpango wa kuhamishia katika jengo la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga lililopo Mtaa wa Bomani katika Manispaa ya Sumbawanga kwa kuwa kuna nafasi kubwa na karibu zaidi na huduma zingine. Tume ya Madini imeweka vifaa vyote vya kisasa ikiwemo mashine ya XRF na Gemological Tool Kit kwa ajili ya kubaini ubora wa madini mara tu yafikapo sokoni.

Pia Mkoa wa Rukwa una vituo viwili vya ununuzi wa madini (mineral buying centres) katika Bandari ya Kabwe na Kasanga kwa ajili ya kuwahudumia wateja wanaoleta madini kutoka nje ya nchi na pembezoni mwa Ziwa Tanganyika.

Aidha, elimu imeendelea kutolewa kwa wadau wa madini hususan wachimbaji wenye leseni za madini yanayoweza kuuzwa sokoni kuongeza zaidi juhudi za kuzalisha madini ili kuvutia wanunuzi wa kutoka ndani na nje ya nchi. Tume ya Madini Rukwa kwa kushirikiana na Vyombo vya Usalama huwapa vibali wachimbaji wadogo wa madini ya vito kupeleka kwenye masoko mengine hususan Dar es Salaam, Arusha na Dodoma ambako kuna wafanyabiashara wakubwa wa madini hayo hapa nchini.

Makundi ya Madini Yanayopatikana Mkoani Rukwa ni yapi?

Sheria ya Madini Sura 123 imeweka madini katika makundi matano (5). Aidha, Mkoa wa Rukwa umebarikiwa kuwa na makundi yote hayo kama ifuatavyo:

Kundi la Madini ya Vito (gemstones); linajumuisha madini yote ya vito: Ruby, Emerald, Aquamarine, Zircon, nk

Kundi la Madini ya Metali (MM); shaba, titanium, dhahabu, bati, chuma, risasi, manganese, n.k

Kundi la Madini ya Viwandani (IM); Helium, Ulanga, Mawe ya Chokaa, Jasi, Kaoline, nk

Kundi la Madini ya Nishati (energy minerals); Coal

Kundi la Madini ya Ujenzi (BM); Mchanga, Kifusi, Mawe ya Nakshi, nk

Jedwali 1: Mwonekano wa Madini katika Maeneo Mbalimbali Mkoani Rukwa

Na

Aina ya Madini

Eneo/Kijiji

Halmashauri

1

Amethyst
Mto Nkomolo, Kasu & Lyazumbi
Nkasi

2

Aquamarine 
Mlombo
Sumbawanga DC

3

Burma Ruby 
Katuka
Sumbawanga MC
Chala & Kantawa
Nkasi

4

Dhahabu
Mto Mfuizi
Kalambo
Mto Mkulwe
Nkasi
Mto Kasulisenga
Nkasi

5

Diatomite, Helium
Bonde la Ziwa Rukwa
Sumbawanga DC

6

Emerald
Sumbawanga
Sumbawanga MC
Mponda
Sumbawanga MC

7

Garnets 
Kantawa, Chala
Nkasi

8

Green Tourmaline 
Chala, Swaila, Lyele na Tambaruka
Nkasi

9

Kaolin 
Kufuata Barabara ya Sumbawanga - Kasanga
Sumbawanga MC & Kalambo

10

Kyanite
Kizi, Chala na Tambaluka
Nkasi

11

Limonite 
Mbuga/ Namwele
Sumbawanga MC

12

Maji Moto
Chemchem ya Mirumba
Kalambo

13

Maji Moto, Thenardite
Chemchem ya Bulongwe
Nkasi

14

Makaa ya Mawe
Muze, Namwele
Sumbawanga DC
Nkomolo
Nkasi

15

Mawe (Aggregates)
Kamita
Sumbawanga MC

16

Mawe ya chokaa
Namwele
Sumbawanga DC

17

Mchanga
Mbarika
Sumbawanga MC

18

Moonstone 
Mkombe Kaskazini mwa Kabwe
Nkasi

19

Piezoelectric Quartz 
Kijiji cha Matala
Nkasi

20

Rare Earth Elements
Mto Kisofi
Kalambo

21

Shaba
Mto Hipanga, Mlima Kasola, Mlima Sensika & Ifumwe
Nkasi
Kasanga na Kapapa
Kalambo

22

Shaba, Nikeli
Mto Malambo
Kalambo

23

Titanium
Kamakanga
Kalambo
Wipanga
Sumbawanga MC

24

Titanium and Zirconium 
Ntemba na Mkwamba
Nkasi

25

Ulanga
Mto Mtose & Mlima Mukwe
Kalambo
Kipala, Mto Luiche & Chulwe
Sumbawanga MC
Tambaruku
Nkasi

26

Zinc 
Kasanga
Kalambo
Kirando
Nkasi

27

Zircon 
Nzombo Kijiji cha Matala.
Nkasi

Mkoani Rukwa Kuna Leseni Ngapi?

Hadi Mwezi Agosti, 2023 Mkoa wa Rukwa ulikuwa na Jumla ya leseni hai zipatazo 249 ambazo zinahusu Utafiti, Uchimbaji wa Kati na Mdogo pamoja na Biashara ya madini kama ilivyoainishwa katika Histogramu.


Kwa mujibu wa takwimu kutoka Ofisi ya Madini Mkoa wa Rukwa uzalishaji wa makaa ya mawe umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka ambapo Kampuni ya Edenville International (T) Ltd kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 Jumla ya tani 7,232.99 za makaa ya mawe yenye Thamani ya Shilingi 1,292,195,403.83 zilichimbwa na kuuzwa ndani na nje ya nchi kutoka kwenye mgodi wake wa Kati uliopo Mkomolo Wiayani Nkasi.

Uwepo wa gesi ya Helium katika Mkoa

Taarifa ya tarehe 19 Februari, 2018 kutoka Ofisi ya Madini ya Kanda-Mpanda ilieleza kuwa mwezi Mei, 2016 Kampuni ya Helium One Ltd ilikuwa inamiliki leseni 8 za utafutaji wa Gesi ya Helium Mkoani Rukwa kupitia kampuni zake tanzu za Helium One (Njozi) Limited, Helium One (Gogota) Limited na Helium One (Stahamili) Limited. Katika kazi ilizokuwa imefanya hadi wakati wa kutoa taarifa ilikuwa imegundua uwepo wa Gesi ya Helium Mkoani Rukwa. Kwa mujibu wa makadirio yaliyofanyika, inaonesha kwamba Gesi hii ipo kwa kiasi kisichopungua futi za ujazo Bilioni hamsini na nne (54bcf).

Hadi kufikia Oktoba, 2023 Mkoa wa Rukwa ulikuwa na jumla ya leseni hai 15 za utafiti mkubwa (Prospecting Licences) wa Madini ya Helium ambapo kati ya hizo sita (6) ni za Kampuni ya Rocket Tanzania Limited ambayo imeanza uchorongaji kwenye kisima cha pili (Mbelele 2) baada ya kukamilisha uchorongaji kwenye kisima cha kwanza (Mbelele 1) katika Kijiji cha Zimba. Aidha kampuni ya Helium One (Njozi) Limited nayo inaendelea kufanya kazi ya uchorongaji upande wa Mkoa wa Songwe lengo likiwa ni kuweza kubaini kiasi halisi kilichopo katika maeneo hayo.

Upatikanaji huu wa Gesi ya Helium utachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Mkoa wa Rukwa na Nchi kwa ujumla.




Ombi kwa Wawekezaji

Fursa za madini mbalimbali yaliyopo Mkoani Rukwa zinapelekea uhitaji mkubwa wa huduma kwa ajili ya wafanyakazi wa viwanda na machimbo ya madini. Huduma za elimu, vyakula, mawasiliano, hoteli za kisasa, kumbi za mikutano, n.k ni kati ya fursa za kupewa vipaumbele ili wananchi kujiongezea kipato.

 

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa