• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Afya Kalambo

imewekwa Tar: October 21st, 2022

SENDIGA: SIJARIDHISHWA NA USIMAMIZI MIRADI YA AFYA KALAMBO

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga amemwelekeza  Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Tano Mwera na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Shafii Mpenda kujitafakari  juu ya namna wanavyosimamia miradi ya ujenzi wa vituo vya afya kutokana na kutokamilika kwa wakati .


Ameagiza hayo   leo (Alhamisi Oktoba 20,2022)  kwa nyakati tofauti alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya sekta ya afya wilaya Kalambo pamoja na kuongea na wananchi kusikiliza kero na shida zao.

Sendiga ametembelea na kukagua vituo vinne ambavyo ni kituo cha afya vya Kanyezi (Milioni 400), Legeza Mwendo (Milioni 700), Mwazye (Milioni 500) na hospitali ya wilaya ya Kalambo (Bilioni 3)  ambavyo kwa pamoja vimeshatumia zaidi ya shilingi Bilioni 4.6 lakini huduma bado hazijaanza kutolewa .

“Sijafurahishwa kabisa kuona vituo vya afya vilivyokaa miaka zaidi ya minne kutokamilika wakati serikali imetoa fedha. Tatizo hapa nimebaini ni viongozi na watendaji wangu kutosimamia miradi hii ya wananchi" alisema Sendiga.

Sendiga aliongeza kusema “ Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi lazima mkae chini na kujitafakari wilaya hii ina nini? , Kalambo kuna shida kubwa  miradi haikamiliki kwa wakati. Siwezi kukubali kuona miradi yenu ikikwama” alisema Mkuu huyo wa Mkoa wa Rukwa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Sunday  Wambura ilionesha kuwa  vituo hivyo vilianza kujengwa mwaka 2018.

Naye Mganga Mfawidhi Kituo cha Afya Legeza Mwendo Dkt. Emanuel Matinda alisema changamoto kwenye miradi ya ya afya ni upatikanaji wa fedha za ndani ya halmashauri kukamilisha kazi ndogo kama za mifumo ya maji taka, umeme na jengo la upasuaji ili huduma kwa wananchi zianze kutolewa.

Naye mkazi wa Matai Mwasulu Abel akizungumza kwenye mkutano wa hadhara alisema vituo vingi vya afya havifanyi kazi icha ya serikali kutoa fedha nyingi hatua inayoleta kero kwa akina mama na watoto.

Mkuu wa mkoa huyo wa Rukwa ametoa agizo kuwa viongozi hao wa wilaya wahakikishe katika kipindi cha siku kumi na nne (14) huduma za afya zianze kutolewa kwenye vituo hivyo vya afya wilayani Kalambo.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa