• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Agizo la Rais Dkt. John Pombe Magufuli latekelezwa kwa asilimia 100 Sumbawanga

imewekwa Tar: November 21st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewapongeza madiwani pamoja na watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kwa kuweza kutekeleza agizo la Rais Dkt. John Pombe Magufuli alilolitoa tarehe 6, Oktoba 2019 alipokuwa katika ziara yake ya siku 3 ambapo aliiagiza halmashauri hiyo kuhamia Laela pamoja na halmashauri nyingine nchini kuhamia katika maeneo yao ya kiutawala.

Amesema kuwa ni watumishi 16 tu kati ya watumishi 165 wa makao makuu ya halmashauri wanaotumia mifumo ya watumishi (LAWSON), mfumo wa mapato LGRCIS), Mfumo wa malipo wa EPICOR, TASAF na Kitengo cha Uchaguzi ndio waliobaki mjini wakisubiri miundombinu hiyo kukamilika katika makao mapya ya halmashauri hiyo katika Mamlaka ya mji mdogo wa Laela.

“Nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kushirikiana na Wadau wengine (Mfano TTCL) ahakikishe anaunganisha Makao Makuu Mapya ya Halmashauri Laela kwenye Mkongo wa Taifa.  Hii itawezesha Mifumo mingine inayotumia Mtandao wa mawasiliano kuweza kufanya kazi kutokea hapa hapa Laela.  Ninamuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha Watumishi ambao bado hawajahamia Laela wawe wamehamia ifikapo tarehe 1 Januari, 2020.” Alisema.

Aidha, ameitaka menejimenti ya halmashauri hiyo kwa kushirikiana na wadau kufanya tathmini juu ya kuwafikia wananchi waliopo mbali na Laela kama vile kutoka katika vijiji vya mfinga, Mwadui, Kalumbaleza wanaokwenda kupata huduma Laela ambao wanatoka umbali wa zaidi ya kilometa 150.

Ameyasema hayo katika kikao cha baraza la madiwani la kwanza kufanyika katika makao makuu hayo mapya ya halmashauri hiyo tarehe 21.11.2019, kikao kilichohudhuriwa na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa, madiwani pamoja na watumishi wa halmashauri.

Awali akitoa taarifa ya maandalizi ya kuhamia katika makao hayo mapya Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule alisema kuwa kitengo cha uchaguzi kimebaki mjini kutokana na kukosekana kwa eneo kubwa la kuhifadhia vifaa vya uchaguzi lakini mara tu uchaguzi utakapopita kitengo hicho kitahamia katika mji wa Laela.

“Kwahiyo Wakimaliza uchaguzi wakiandaa ile taarifa tutahakikisha nao wanahamia haa Laela, Watu wa Fedha na watu wa Utumishi wanawasiliana na watu wa TTCL ili mokongo ule wa taifa uweze kupatikana hapa Laela na zile huduma zao ziweze kuhamia hapa Laela, kwa ujumla shughuli zinaenda vizuri na wananchi wanaendelea kuhudumiwa vizuri hapa Laela,” Alisema.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Apolinari Macheta alisema kuwa watumishi wa halmashauri hiyo walikuwa wakishiriki usafi wa Jumamosi ya mwisho wa mwezi katika eneo ambalo halikuwa la kwao na pia walikuwa wakichangia maendeleo katika maeneo ambao sio ya kwao.

“Tulichelewa sana na ni maamuzi ambayo yangefanyika hata huko nyuma tungeweza kuwa parefu zaidi lakini tunakushukuru sana kwa namna mji wetu wa Laela ulivyo hautofautiani na mji wa sumbawanga na hata kama ni changamoto ni za kawaida haziwezi kufanana na za wengine kwakweli tunaonekana tuko mjini.” Alisema.

Wakati akitoa neno la Shukurani mbunge wa jimbo la Kwela Mh. Ignus Malocha alisema kuwa yeye ndio wa kwanza kutangulia kwani ofisi yake ilikuwa ya kwanza kabla ya Mkurugenzi kuhamia katika mji huo baada ya wiki mbili tu tangu Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutoa agizo hilo, hivyo alimshukuru mkuu wa mkoa kwa kusimamia zoezi hilo la utekelezaji wa agizo la Rais.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa