• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

AWEKEZAJI RUKWA WATAKIWA KUONGEZA UZALISHAJI WA CHAKULA CHENYE VIRUTUBISHO KUPUNGUZA UDUMAVU

imewekwa Tar: August 30th, 2024



Serikali Mkoani Rukwa imewataka wawekezaji katika viwanda vya uzalishaji wa chakula kuongeza uzalishaji wa chakula chenye virutubisho muhimu ili kupunguza changamoto ya udumavu inayotokana na lishe duni.

Hayo yamesemwa wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai 2023- Juni 2024 kilichofanyika tarehe 29 Agosti 2024 katika ukumbi wa RDC ulioko katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.


Kikao hicho kilichoongozwa na Mheshimiwa Peter Ambrose Lijualikali kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere kimeshauri kila Halmashauri kuweka mkakati maalum wa kuongeza idadi ya viwanda hatua itakayoongeza kiwango cha uzalishaji wa chakula chenye virutubisho. 


Mheshimiwa Lijualikali ameeleza kuwa, kuanzishwa na kuimarishwa kwa viwanda vinavyochakata chakula vyenye virutubisho ni hatua muhimu katika kuboresha afya na ustawi wa wananchi, hasa watoto na wanawake wajawazito ambao wako katika hatari kubwa ya kukumbwa na matatizo udumavu.


Wajumbe wa Kikao hicho wameshauri kuwa mkakati huo ushirikishe sekta ya kilimo, viwanda, afya, na wadau wa maendeleo, kwa lengo la kujenga uwezo wa ndani wa uzalishaji na usambazaji wa chakula vyenye virutubisho.

Mheshimiwa Lijualikali ameeleza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wawekezaji na wadau mbalimbali ili kuhakikisha mkakati huo unafanikiwa na unaleta matokeo yanayotarajiwa ikiwa ni sehemu ya juhudi ya Mkoa wa Rukwa kuhakikisha kuwa mkataba wa lishe unatekelezwa kikamilifu.

Matangazo

  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • MATOKEO YA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 November 05, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MKUU WA MKOA WA RUKWA ATOA WITO KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 27, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI RUKWA LAPOKEA MAGARI MATATU YA KISASA KUIMARISHA SHUGHULI ZA UOKOAJI

    October 27, 2025
  • SERIKALI YATOA PIKIPIKI KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WA HALMASHAURI RUKWA

    October 24, 2025
  • MBIO ZA MWENGE ZAENDELEA KALAMBO RUKWA, MIRADI YA MAENDELEO YAENDELEA KUMULIKWa

    September 30, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa