• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Baada ya miaka 6 bila ya kutumika soko la samaki Kasanga laundiwa timu kuchuguza ubadhirifu.

imewekwa Tar: November 15th, 2018

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amwemuagiza katibu tawala wa Mkoa wa Rukwa kuhakikisha anaunda timu kwaajili ya kufanya uchunguzi juu ya matumizi ya fedha iliyotumika kwenye ujenzi wa soko hilo uliokamilika mwezi Novemba mwaka 2011 na kuzinduliwa mwaka 2012 na aliyekuwa makamu wa rais Dkt. Gharib Bilal.

Mh. Wangabo amesema kuwa hali ya soko ilivyo ni tofauti na thamani inayotajwa ambayo ilitumika kwaajili ya ujenzi wa soko hilo na tangu kuzinduliwa kwake halijaanza kutumika kama ilivyotarajiwa ambapo walengwa ni wakazi wapatao 35,205 waishio mwambao wa ziwa Tanganyika.

“Bilioni moja nukta imekwisha lala hapa, RAS unda timu ije ifanye tathmini ya fedha iliyotumika hapa, hiyo ni fedha ya serikali na tunakatisha tamaa wenzetu wanaotusaidia Jumuiya ya Ulaya wametoa zaidi ya milioni 700 na wengine MIVRAF wametoa milioni karibui 300, hawa wawili tu ni bilioni moja jumlisha milioni 100 za halmashauri bado hapa mahali hapajakamilika na mapungufu yapo,” Alifafanua.

Halikadhalika alieleza kuwa mfumo wa meko yaliyopo katika soko hilo sio rafiki wa mazingira hivyo aliwataka watakaotumia soko hilo wafikirie namna ya kutengeneza mkaa mbadala kwa kutumia makaa ya mawe yanayopatikana kwa wingi katika kijiji cha Nkomolotu, Wilayani nkasi mkoani humo.

Wakati akisoma taarifa ya soko hilo afisa uvuvi wa halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Nicholas Mrango alisema kuwa wananchi wa mwambao huo wana fursa ya kuvua samaki kwa wastani wa tani 167,000 kwa mwaka na kuongeza pato la halmashauri na serikali kuu na kutaja malengo ya mradi huo na changamoto zake.

“Malengo ya mradi ni kuboresha hali ya uchumi wa wananchi, kupata wanunuzi wa samaki wa uhakika ndani nan je ya nchi lakini ili soko lianze kutumika linahitaji miundombinu ya umeme, chumba cha kukaushia samaki, mtambo wa kugandisha barafu, meza za kuuzia samaki na chanja za kuanikia ili kukidhi kiwango cha kimataifa,”Alibainisha.

Soko kuu la samaki hao ni pamoja na ndani ya wilaya ya Kalambo, mkoa wa Rukwa kwa ujumla, Mikoa ya Mbeya, Iringa,Njombe na Ruvuma na pia nchi za jirani za Zambia, Demokrasia ya Watu wa Congo, Rwanda na Burundi.  

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa