• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Bilioni 27 zatumika Kuboresha Barabara Rukwa

imewekwa Tar: March 1st, 2022

BILIONI 27 ZATOLEWA KUBORESHA BARABARA ZA RUKWA- RC MKIRIKITI

Na. OMM Rukwa.

Zaidi ya shilingi Bilioni 27.5 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa barabara zilizo chini ya Wakala za TANROADS na TARURA katika mwaka wa fedha 2021/2022 ikiwa ni ongezeko la kibajeti mara mbili zaidi ya lile la awali kwa mwaka fedha uliopita.

Kutolewa kwa fedha hizo kunatajwa kuwa ni moja ya mafanikio makubwa ya serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan tangia aingie madaraka takribani mwaka mmoja hadi sasa.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha 40 Bodi ya Barabara mkoa hii leo (28.02.2022) mjini Sumbawanga, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti amesema fedha hizo tayari zinaendelea kutekeleza miradi ya barabara kwenye maeneo mbalimbali mkoani humo.

“Nichukue fursa hii kuipongeza serikali yetu inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutupatia fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya barabara zetu ambapo maendeleo makubwa yanaonekana kote “alisema Mkirikiti.

Mkuu huo wa Mkoa aliongeza kusema kqti ya fedha hizo shilingi Bilioni 15.2 ni kwa ajili ya barabara za Tanroads na Bilioni 12.3 ni kwa ajili ya barabara za Tarura.

Mkirikiti aliwataka wajumbe wa kikao hicho kufanya tathmini ya kina juu ya matumizi ya fedha hizo za barabara kwa kuwa zimetolewa na serikali kwa lengo la kuboresha barabara hususan za vijijini ili zichochee ukuaji wa uchumi .

“Fedha hizi ni zaidi ya mara tatu ya makusanyo ya halmashauri zetu zote nne. Makusanyo ya ndani ya halmashauri zetu ni Bilioni takribani 9 katika mwaka 2021/22” alisema Mkirikiti.

Aidha, Mbunge wa Kalambo Josephat Kandege aliomba serikali kufanya udhibiti na kulinda eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mpya wa ndege Kisumba ili wananchi wasilivamie na kwa kilimo na makazi.

Akiwasilisha  taarifa ya utekelezaji kazi za barabara kuu za mkoa kwa mwaka 2021/22 na mpango na bajeti kwa mwaka 2022/2023 Meneja wa Tanroad Mkoa wa Rukwa Mhandisi Mgeni Mwanga alisema asilimia kubwa barabara za mkoa za lami na changarawe zote zilikuwa na hali nzuri.

Mhandisi  Mwanga  alisema Tanroad inasimamia mtandao wa barabara zenye urefu wa kilometa 1,250.2 ambapo barabara kuu zina urefu wa kilometa 415 kati ya hizo za lami ni (298.35 km) na changarawe (117.51 km) na  barabara za mkoa  zina jumla ya kilometa 834.98 kati hizo za lami ni (76.8 km) na za changarawe ni (758.1 km) .

Mhandisi Mwanga alisema katika mwaka 2022/2023 bajeti ya matengenezo kupitia Mfuko wa Barabara inayotarajia kupitishwa na Bunge ni shilingi Bilioni 13.81 ambapo jumla ya madaraja 32 katika barabara kuu na madaraja 62 katika barabara za mkoa yatajengwa na kukarabatiwa.


Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa