• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

BILIONI 55.9 ZALIFUNGUA ANGA LA SUMBAWANGA

imewekwa Tar: May 5th, 2023

BILIONI 55.9  ZALIFUNGUA ANGA LA SUMBAWANGA

Mkataba wa ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Sumbawanga umetiwa saini kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi na Kampuni ya Beijing Construction Enginering Limited ya China.

Hafla ya kusaini Mkataba huo imefanyika leo tarehe 29 Aprili 2023 huku ukishuhudiwa na Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa ambaye alikuwa mgeni rasmi, wengine ni Mhe. Queen Cuthbert Sendiga ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Mhe.  Sultan Saleh Seif, Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini Mhe. Aeish Hillal Khalfan, Katibu Tawala  wa Mkoa wa Rukwa Bw. Gerald Kusaya, Wakuu wa Wilaya  na Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Rukwa .

Akizungumza na mamia ya wananchi waliokusanyika katika eneo la uwanja wa ndege unaotarajiwa kukarabatiwa Mhe. Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi amemshukuru na kumpongeza Mhe. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutafuta fedha kutoka Benki ya Uwekezaji ya Ulaya kwa ajili ya ukarabati wa kiwanja hicho cha ndege.

Amesema miundombinu ya uwanja itaruhusu ndege kutua na kupaa usiku na mchana na kwamba uwanja utahudumia na kuunganisha ukanda wa magharibi na mikoa mingine. Mkataba wa ujenzi ni wa miezi  kumi na nane na unatarajiwa kukamilika Oktoba 2024. Urefu wa njia ya kurukia ndege unatarajiwa kuongezeka kutoka mita 1560 mpaka mita 1750 na upana kubakia mita 30 kama ilivyokuwa awali. Gharama ya Mkataba wa kazi hiyo ni shilingi  Bilioni 55.9 .

Aidha Mhe. Prof. Mbarawa amewaagiza Tanroads na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kumsimamia Mkandarasi ili kazi ifanyike kwa ufanisi huku akiwaomba wananchi kutoa ushirikano unaohitajika.

Akitoa salamu za Mkoa wa Rukwa Mhe. Queen Cuthbert Sendiga amempongeza, kumshukuru na kumkaribisha Mhe. Prof. Mbarawa Mkoani Rukwa. Ametumia nafasi hiyo kueleza kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya awamu ya Sita katika kipindi cha miaka miwili.

Wakitoa shukrani zao kwa Serikali kwa niaba ya wananchi wa Sumbawanga, Mbunge wa Sumbawanga Mjini na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga wamewaomba na kuwasihi wananchi kuendelea kuiunga mkono Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan huku wakiendelea kuwaombea viongozi wote wa Serikali ili waweze kuwatumikia bila kuchoka.


Matangazo

  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAZAZI WAPATIENI WATOTO ELIMU KUHUSU HEDHI SALAMA

    June 02, 2023
  • WAWEKEZAJI KUTOKA ZAMBIA WAVUTIWA NA BANDARI MKOANI RUKWA

    May 28, 2023
  • MRADI WA MAJI WAZINDULIWA KISA

    May 15, 2023
  • ZAHANATI YA MPONA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA YAZINDULIWA

    May 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa