• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Bodi ya Barabara Rukwa

imewekwa Tar: October 11th, 2022

RC SENDIGA:  BILIONI 29 KUBORESHA BARABARA ZA TARURA NA TANROAD

 

Na. OMM Rukwa

Serikali katika mwaka wa fedha 2022/23 itatumia shilingi Bilioni 29.43 kwa ajili ya kazi za matengenezo na madaraja kwa Wakala wa Barabara (TANROAD) na TARURA kwa mkoa wa Rukwa ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga amebainisha hayo leo (11.10.2022) mjini Sumbawanga wakati Akifungua kikao cha 41 cha Bodi ya Barabara cha kwanza kwa mwaka 2022/2023 ambapo ametoa wito kwa wananchi kutunza miundombinu hiyo.

Sendiga aliongeza kusema kati ya fedha hizo Bilioni 29.43 tayari hadi kufikiwa Septemba 2022, TANROAD imepokea shilingi Bilioni 16.65 na TARURA imepokea   shilingi Bilioni 12.78 na kuwa kazi za ujenzi na ukarabati zinaendelea.

Taarifa ya mkoa inaonesha kuwa katika mwaka wa fedha 2021/22 hadi kufikiwa Juni 2022 wakala zote mbili zilipokea jumla ya shilingi Bilioni 27.56 kwa ajili ya kazi za matengenezo ya barabara.

“Ni imani yangu kuwa fedha hizi zilizotolewa kwa ajili ya matengenezo ya barabara katika mkoa wetu wa Rukwa zitawanufaisha wananchi wote, wakandarasi wakubwa na wadogo na vikundi vya akina mama kwa kuwapa kazi za mikono ili kukuza kipato cha kaya” alisisitiza Sendiga.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa agizo la Rais pamoja na agizo la Katibu Mkuu wa CCM la kupunguza matuta kwenye barabara ya Tunduma –Sumbawanga, Katibu Tawala Msaidizi wa Miundombinu, Mhandisi Daudi Sebyiga alieleza kuwa TANROAD imetenga fedha na kuwa kazi ya kumtafuta mzabuni kwa ajili ya kazi hiyo imeanza Septemba 2022.

Katika hatua nyingine Mwakilishi wa Meneja wa TANROAD Mkoa wa Rukwa Mhandisi Suzana Lucas alisema hadi Septemba 2022 hali ya barabara kuu za lami asilimia 76 sawa na ambazo ni kilometa 226  ni nzuri, na zile cha changarawe asilimia 24.68 sawa na kilometa 29 ni nzuri .

Aidha, Mhandisi Suzana aliongeza kusema  asilimia 92 ya barabara za mkoa zenye lami sawa na kilometa 70 ni nzuri huku kilometa 645 za changarawe sawa na asilimia 85 ni za wastani na zinapitika wakati wote wa mwaka.

Nae Meneja wa TARURA mkoa wa Rukwa Mhandisi Samson Kalesi alisema hadi kufikia Juni 30, 2022, mkoa ulikuwa umeingia mikataba 49 na wakandarasi yenye jumla ya shilingi 11,288,000,000.00 kwa ajili ya kutekeleza kazi mbalimbali za ujenzi na matengenezo ya barabara, madaraja na makalavati.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa