• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

CCM

imewekwa Tar: August 31st, 2021

“HAKUNA UBINAFSI KWENYE FEDHA ZA SERIKALI”- RC MKIRIKITI 


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa Rainer Lukala amewaagiza Viongozi na Watendaji wa serikali kote mkoani Rukwa kutumia vizuri fedha za umma ili zitekeleze miradi ya maendeleo hatua itakayoondoa kero.

Amebainisha kuwa wananchi wana imani na serikali yao ambayo imeahidi kupitia Uchaguzi  Mkuu wa mwaka 2020 kutatua kero za wananchi hususan huduma za miundombinu, maji, elimu na afya ili maendeleo yapatikane.

Agizo hilo amelitoa  (21.08.2021) wakati akifungua kikao  cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Rukwa kuhusu kupokea taarifa ya serikali ya Utekelezaji wa Ilani  Uchaguzi iliyowasilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa  mjini Sumbawanga.

“Lengo letu Chama cha Mapinduzi ni kuhimiza matumizi sahihi ya fedha za umma na pale tutakapobaini ubadhirifu na matumizi mabaya tutashauri serikali kuchukua hatua kwa watendaji watakaohusika” alisema Lukala

Kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi aliongeza kusema sekta za miundombinu chini ya Tarura na Tanroads na sekta za Mifugo, maji bado zina changamoto hivyo kuhitaji usimamizi wa watendaji wa serikali kwani fedha nyingi zinapelekwa huko lakini bado wananchi wana kero.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ,Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti amebainisha kuwa katika kipindi cha mwezi Novemba 2020 hadi Juni 2021 mkoa ulikusanya jumla ya Shilingi Bilioni 13.8 za kodi ya ndani ,kodi za forodha na ushuru wa mauzo kati ya lengo kukusanya Shilingi Bilioni 10.5 sawa na asilimia 131.

Mkirikiti alisema mkoa umejipanga kusimamia kikamilifu matumizi sahihi ya fedha za umma kwa kuzingatia sheria na kanuni za matumizi ya fedha za serikali ambapo watekelezaji wakuu ni watendaji wote wa taasisi na mashirika ya umma mkoani.

“Hakuna ubinafsi kwenye fedha za serikali. Ndio maana zinaitwa fedha za umma hivyo Watendaji wa taasisi na mashirika ya umma hakikisheni zinasimamiwa kwa usawa na uwazi ili ziwafikie wananchi wote kwenye miradi iliyopangwa” alisema Mkirikiti

Kwa upande makusanyo ya halmashauri Mkuu huyo wa Mkoa alisema katika kipindi cha Julai 2020 hadi Juni 2021 zilifanikiwa kukusanya Shilingi Bilioni 8.4 kati ya lengo la kukusanya Bilioni 9.4 sawa na asilimia 88.8 ya makisio ya mwaka.

Mkirikiti alibainisha mafanikio kadhaa yaliyopatikana katika Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya Mwaka 2020-2025 ambapo kwa sekta ya kilimo alisema tija ya uzalishaji zao la mahindi kwa wakulima wadogo imeongezeka toka tani 2.4 kwa hekta mwaka 2020 hadi tani 2.5 mwaka 2021

Kuhusu sekta ya Uvuvi mkoa wa umefanikiwa kutoa elimu juu ya matumizi ya zana bora za Uvuvi kwa wavuvi 487 na pia kiwanda kikubwa cha kuchakata mazao ya samaki kimeanzishwa.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa ametoa rai kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi kusaidia kutoa elimu kwa wananchi kuhusu maandalizi ya sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika nchini mwaka 2022.

Mwisho.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa