• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Chanjo Polio

imewekwa Tar: May 18th, 2022

WATOTO 217,674 RUKWA KUPATA CHANJO YA POLIO

Na. OMM Rukwa

Mkoa wa Rukwa umezindua zoezi la utoaji chanjo ya polio kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano ambapo imelenga kuwafikia watoto 217,674 katika wilaya za Sumbawanga, Nkasi na Kalambo.

Mkuu wa Mkoa huo Joseph Mkirikiti leo (18.05.2022) amezindua kampeni hiyo katika kituo cha afya Mazwi kilichopo Manispaa ya Sumbawanga na kutoa rai kwa wazazi kuwapeleka watoto kupata chanjo hiyo ambayo itawakinga dhidi ya ugonjwa wa kupoza.

“Wazazi jitokezeni kupeleka watoto kwenye vituo vya afya ili wapate chanjo hii ya polio ambayo ni salama na itawakinga dhidi ya ugonjwa wa kupoza. Madhara ya polio ni hatari, hivyo tuwalinde watoto wetu ili waendelee kuwa salama” alisema Mkirikiti.

Mkirikiti alieleza kuwa wazazi wawe mabalozi kwa wenzao wenye watoto chini ya miaka mitano kuhamasisha washiriki zoezi hilo ambalo linafanyika kote katika vituo vya afya mkoani Rukwa.

Akitoa taarifa ya kampeni hiyo kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa, Mratibu wa Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto mkoa wa Rukwa Asha Izina alisema mkoa umepanga kuchanja watoto walio na umri chini ya miaka mitano wapatao 217,674 kutoka katika halmashauri nne za Rukwa.

Mratibu huyo aliongeza kusema maandalizi yamekamilika ambapo tayari watoa huduma 504 watakaoshiriki zoezi la uchanjaji wametakiwa mafunzo na kuwa mkoa umepokea chanjo dozi 250,320 na vifaa vingine.

Naye Mganga Mkuu wa Manispaa ya Sumbawanga Dkt. Sebastian Siwale alisema polio ni ugonjwa unaosababisha watoto kupoza hivyo akitoa wito kwa wazazi na walezi kuwapeleka watoto kwenye vituo vya afya kupata chanjo hii muhimu.

Dkt. Siwale aliwatoa hofu wazazi kuwa chanjo hii haina madhara kwani imekuwa ikitolewa siku zote kwenye kliniki kwa watoto lakini kutokana na nchi jirani ya Malawi kuwa na mlipuko wa ugonjwa huu, Serikali imelazimika kuendesha kampeni hii ili kuwafikia watoto wengi zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari mmoja wa wazazi aliyejitokeza kwenye zoezi hilo Bahati Juma mkazi wa Sumbawanga alisema baada ya kusikia matangazo kwenye redio ndipo akaamua kumpeleka mtoto wake ili apate chanjo ya polio ili asije ambukizwa ugonjwa huo.

Kampeni ya polio imeanza leo na itachukua muda wa siku nne hadi tarehe 21 Mei mwaka huu itakapohitimishwa katika halmashauri za Sumbawanga Manispaa, Sumbawanga vijijini, Kalambo na Nkasi,

Mwisho.

Matangazo

  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Kodi kwa Maendeleo September 15, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chanjo Polio

    May 18, 2022
  • NFRA

    May 11, 2022
  • Vyama vya Ushirika

    May 05, 2022
  • Eng. Kundo: Nimeridhishwa na Zoezi la Anwani za Makazi Rukwa

    April 27, 2022
  • Angalia Zote

Video

RC Mkirikiti akabidhiwa Ofisi Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0764902066

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa