• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

DC Kalambo awataka wasichana kuanza kijilinda wenyewe kupunguza mimba za utotoni

imewekwa Tar: October 11th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Julieth Binyura amewataka wasichana wa shule za msingi na sekondari kuhakikisha wanaanza kujilinda wenyewe kwa kutojiweka na kujihusisha na mazingira tatanishi wanapotoka shuleni na badala yake waendelee kusaidi kazi za nyumbani na kujisomea wakiwa nyumbani.

Ameyasema hayo katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga huku akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo kama mgeni rasmi wa maadhimisho hayo.

Pia ametoa wito kwa wazazi na walezi mkoani humo kuhakikisha wanawalinda watoto wa kike lakini ili kupunguza vitendo vya ukatili amewaomba wazazi kushirikiana kujenga mabweni ili kuwahakikishia ulinzi watoto hao.

“Kauli mbiu inasema tuwalinde watoto wa kike, ni kweli tuwalinde kwani tusipofanya hivyo, tutahatarisha nchi yetu na kuhatarisha dunia nzima kwa watoto kukosa maadili mazuri, maadili yanatoka kwetu wazazi, nawaomba wananchi qwote wa Mkoa wa Rukwa tuwalinde watoto wetu wanapokuwa mashuleni na majumbani,” Alisisitiza.

 Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasmi mwanafunzi Amina Suleiman amesema kuwa ingawa katika familia nyingi hawatoi kipaumbele cha kuwasomesha watoto wa kike lakini imeshuhudiwa mara kadhaa watoto hao wa kike ndio wanaowalea wazazi.

“Utafiti uliofanywa na wadau mbalimbali wa haki za watoto, umebaini kuwa hali duni ya kiuchumi ya wazazi wengi umechangia watoto wao wa kike kukatisha masomo kwa lengo la kuwaoza au kuwapeleka kufanya kazi za ndani ili waweze kuwasaidia kipato kidogo wanachokipata,” Alibainisha

Halikadhalika aliongeza kuwa shirikala maendeleo ya wasichana linasema kuwa wasichana milioni 39 kati ya umri wa miaka 11 hadi 15 hawamalizi masomo yao.

Kuanzia Julai 2017 hadi Mei 2018 jumla ya wanafunzi 149 wamepata ujauzito katika mkoa wa Rukwa, huku wanafunzi wa shule ya msingi wakiwa 59 na sekondari ni 98. Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na watendaji wa kata kufikisha kesi hizo polisi na mahakamani kwa hatua Zaidi na mapaka sasa matukio yote 149yameripotiwa polisi na 7 yapo mahakamani.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa