• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

DC Mtanda awatahadharisha kinababa wenye tabia ya kunyonya maziwa ya mama

imewekwa Tar: August 1st, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda amewatahadharisha kinababa wenye tabia ya kunyonya maziwa ya kinamama wanaonyonyesha kwani hicho ni chakula maalum kwaajili ya mtoto aliyezaliwa na yeyote anayefanya hivyo anadhulumu haki ya mtoto ambaye hutegemea maziwa ya mama kwa muda wa miezi sita bila ya kula chakula cha aina yoyote.

Amesema kuwa kazi kubwa ya kinababa ni kuwawezesha kinamama kupata lishe bora ili wawe na afya thabiti kutoa maziwa ya kutosha na kuweza kuwanyonyesha watoto wao na kuongeza kuwa katika mkoa wa Rukwa asilimia 81 ya watoto wenye umri chini ya miezi sita wanalishwa vyakula vingine vya ziada, jambo ambalo halikubaliki kwa maendeleo ya mtoto.

“Ujumbe wa Leo ni kwamba watoto wadogo chini ya Miezi Sita ndio wanaotakiwa kunyonyeshwa, kwahiyo kinababa na wao wenye kupenda maziwa ya baba waache kwasababu hicho sio chakula chao ni lishe kwa watoto wachanga, tusidhulumu haki za watoto za unyonyeshaji, tuache tabia ya kunyonya maziwa ya mama kwa wasiohusika,” Alisisitiza.

Aidha alisema kuwa tafiti zinaonesha kuwa asilimia 17 ya watoto wenye umri chini ya miezi 6 wananyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila kupewa kinywaji au chakula kingine kama inavyoshauriwa na Shirika la Afya Duniani. Hii ina maana kuwa asilimia 83 ya watoto wenye umri huo hawanyonyeshwi ipasavyo.

Mh. Mtanda aliyasema hayo katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji kimkoa katika Kijiji cha Kisumba, kilichopo Wilaya ya Kalambo akimwakilisha aliyetakiwa kuwa mgeni rasmi wa uzinduzi huo Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Albinus Mgonya aliisifu timu ya afya ya Mkoa kwa kuwezesha kufanyika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji katika Kijiji cha kisumba kutokana na Kijiji hicho kuwa na kinamama wengi wanaonyonyesha.

“Katika Kijiji hiki Mheshimiwa mgeni rasmi kuna Kaya 1300, na kwa takwimu ambazo tunazo kupitia idara yetu ya afya kinamama wanaonyonyesha watoto katika Kijiji hiki cha Kisumba ni 234, hivyo utaona kwamba tumekuja kuhakikisha kuwa ujumbe huu unafika kwa wadau kwa njia muafaka,” Alieleza.

Halikadhalika alisema kuwa maadhimisho hayo yankwenda sambamba na utekelezaji wa mradi wa Lishe Endelevu unaolenga kuongeza idadi ya watoto wenye umri kati ya miezi 6 – 23 kuhakikisha kwamba wanapata vyakula vyenye mchanganyiko sahihi na kusisitiza kuwa ni muhimu kinababa kushiriki katika maadhimisho hayo ili wawe msaada mkubwa kwa kinamama.

Wakati akitoa neno la Shukrani Meneja wa Mradi wa Lishe Endelevu Ali Omar alishukuru ushirikiano anaoupata kutoka serikalini na kuwasisitiza kinamama kuwa unyonyeshaji wa maziwa ya mama huchangia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha afya, kulinda uhai na maisha ya mtoto.

Asilimia 67 ya watoto wa umri kuanzia miezi 6 – 23 wanapewa vyakula ambavyo havina mchanganyiko wa kutosha, yaani mlo usiokamilika, hali inayodhihirisha kuwa, taratibu duni za ulishaji watoto ni mojawapo ya sababu za utapiamlo katika Mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa