• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

DC Nkasi asisitiza kufikishwa elimu ya UKIMWI kwenye vitongoji.

imewekwa Tar: December 1st, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda ameisisitiza idara ya maendeleo ya jamii wanaoshughulikia usambazaji wa elimu ya Ukimwi katika Mkoa na Halmashauri kuhakikisha elimu ya UKIMWI inawafikia watu wa makundi yote hadi katika ngazi ya vitongoji.

Amesema kuwa wananchi wa vijijini ndio wenye kuihitajia zaidi elimu hiyo kuliko wa mjini ambapo kuna utitiri wa vyombo vya habari na ofisi nyingi zinazoshughulika na kutoa huduma hiyo kuliko vijijini ambapo upatikanaji wa taarifa na elimu hiyo ni changamoto.

“Niataendelea kuwasisitiza watu wa maendeleo ya jamii wakishirikiana na masirika mbalimbali yanayotoa elimu ya UKIMWI kuhakikisha kuwa wanawafikia wananchi wa vijijini, kwani hadi hii leo kuna watu huko vijijini hawajui matumizi ya kondomu na matokeo yake kondomu hiyo moja inatumika zaidi ya mara mbili, mtu anifua na kuitumia tena,” Mh. Mtanda alisisitiza

Ameyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika Kimkoa katika Viwanja vya shule ya Msingi Ndua, Kizwite, Manispaa ya Sumbawanga aliyemuwakilisha mgeni rasmi wa maadhimisho hayo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo.

Aidha amewatahadharisha wananchi kuwa kupata UKIMWI haina maana kuwa ni marehemu mtarajiwa bali yeyote atakayeupata ugonjwa huo azingatie ushauri wa wataalamu na kufuata masharti ili aweze kuendelea kuishi na kusaidia kujenga taifa letu.

Kwa upande wake Deo Crispin Mlori aliyeishi na UKIMWI kwa miaka 27 amesema kuwa kwa kufuata masharti wamekuwa wakiishi vizuri yeye na mke wake ambao hadi hivi sasa wana watoto wanne wanaowasomesha kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.

Awali akisoma risala afisa maendeleo ya jamii Mkoa Aziza Kaliatila amesema kuwa kiwango cha maambukizi kwa mkoa wa Rukwa ni asilimia 6.2, kiwango ambacho kipo juu ya maambukizi ya UKIMWI kitaifa.

“Jumla ya wananchi 308727 wamejitokeza kupima VVU ikiwa wanawake 167623 na wanaume 141104 kwa mwaka2016/2017. Waliokutwa na maambukizi ni 4620 Wanawake 2602 Wanaume 2018.” Aziza alifafanua.

Ameongeza kuwa Mkoa umekuwa ukifanya uhamasishaji wa mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kutumia gari la sinema Jumla ya vijiji 89 na Kata 36 zimefikiwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

“Mkoa pia umeendelea kutoa misaada ya kibinadamu kwa vikundi WAVIU vya 34 kwa gharama ya Shilingi 43,000,000 na watoto yatima wapatao 611 wamelipiwa  ada za shule jumla ya Shilingi 24,070,000.” Amesema.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa