• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

DC Sumbawanga awaonya kinamama wanaowanyesha pombe vichanga

imewekwa Tar: August 2nd, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule amewaonya kinamama wenye tabia ya kuwanywesha watoto wachanga pombe pindi waliapo kwa lengo la kuwanyamazisha walale ili wao waendelee na shughuli nyiungine za kujitafutia kipato.

Amesema kuwa mambo hayo mara nyingi hujitokeza kipindi cha msimu wa kilimo ambapo mama huenda na mwanawe shambani na pindi anapolia humnywesha mtoto huyo pombe ili apate kuendelea kulima bila ya bughudha yoyote.

“Kwenye mazingira yetu tumeshuhudia watoto wanalishwa vyakula vya ziada lakini hasa pombe, wakati wa masika tumeshuhudia akinamama wanashughuli nyingi za kilimo na kutokana na hizo shughuli hawapati nafasi ya kuandaa chakula cha watoto, na kwavile wanatakiwa kulima basi wanakwenda na pombe shambani, uwongo…kweli? Mtoto akipiga kelele akitaka kunyonya, unamtandika pombe analala chini ya mwembe, hiyo haikubaliki,” Alisisitiza.

Ameongeza Aslimia 19 ya watoto wenye umri chini ya miezi sita wananyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila ya kupewa kinywaji ama chakula kingine kama inavyoshauriwa na wataalamu ikiwa na maana kuwa asilimia 81 ya watoto wenye umri huo hawanyonyeshwi ipasavyo na kuchanganyiwa chakula hivyo kuwaweka katika hatari ya utapiamlo na magonjwa yanayopatikana katika utaratibu usiofaa.

Ameyasema hayo alipokuwa akizindua wiki ya unyonyeshaji akimuwakilisha mgeni rasmi wa uzinduzi huo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, shughuli iliyofanyika kimkoa katika viwanja vya shule ya msingi Mkomanye, kijiji cha Muze, Wilayani Sumbawanga.

Mmoja wa akinamama waliohudhuria kwenye uzinduzi huo Kalista Mpasa laisema kuwa miongoni mwa sababu zinazosababisha wanawake kushindwa kuwanyonyesha watoto wao kwa muda unaotakiwa ni kutokana na tabia za uasherati na hatimae watoto hao kupata udumavu na kuipa serikali mzigo wa kuwalea.

Nae Efrozina Luheka mama mwenye kitoto kichanga amesema kuwa anaunga mkono serikali kwa kufanya juhudi za kuhakikisha wanawaelimisha kinamama juu ya umuhimu wa kuwanyonyesha watoto na hatimae kuwa na afya njema kuwajali na kupunguza wimbi la watoto wa mtaani.

Kwa upande wake meneja wa mradi wa uzazi salama mkoa wa Rukwa unaofadhiliwa na Global Affairs Canada Dkt. Noah Mwaipyana ameeleza sababu kadhaa wanazozitumia kinamama kukwepa kuwanyonyesha watoto kwa muda unaotakiwa hukunakisisitiza elimu kusambazwa zaidi.

“Kuna sababu nyingi ambazo kinamama wanazitumia kukwepa kunyonyesha watoto, mojawapo ni kuwa na shughuli nyingi na wengine wakisema kuwa maziwa hayatoki na wakati mwingine ni kukosekana kwa uelewa, mtoto akilia wakati mwingine wanachukulia kwamba maziwa hayatoshi na wanakwepa kunyonyesha, sisi tunaingilia kati ili kuhakikisha kwamba mama akishajifungua anapata lisha ya kutosha,” Alisema Dkt. Mwaipyana.

Kwa Mkoa wa Rukwa asilimia 33 tu ya watoto wenye umri wa kuanzia miezi 6 hadi 21 wanapewa vyakula vya mchanganyiko vinavyokidhi mahitaji ya lishe na asilimia 67 ya umri huo wanapewa umlo usiokamilika, na asilimia 12 tu wenye umri wa miezi 6 hadi 23 wanapata chakula cha kiwango cha chini cha ulishaji kama inavyoshauriwa na wataalamu wetu.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa