• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Gereza Mollo

imewekwa Tar: November 1st, 2021

DHANA YA MAGEREZA KUJITEGEMEA IBORESHE MIRADI

 

Jeshi la Magereza nchini limepongezwa kwa kubuni utaratibu mzuri wa kujiendesha kimapato kupitia miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa nyumba bora kwa gharama nafuu.

Pongezi hizo zimetolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti wakati alipozindua mradi wa nyumba za kuishi askari na mradi wa maji kwenye gereza la kilimo Mollo wilaya ya Sumbawanga.

Mkirikiti alifurahishwa kuona mradi wa nyumba ya kuishi familia mbili iliyojengwa kwa shilingi Milioni  Hamsini na Tano na aliwapongeza kwa kutekeleza dhana ya Magereza Kujigemea kwa kuwa inaongeza tija kwa mkoa kupitia miradi inayotekelezwa.

“Kama Magereza imeweza kujenga nyumba moja ya familia (Two in One) kwa gharama ya shilingi Milioni 57, huu ni mfano mzuri wa ubunifu. Wito wangu Halmashauri za Rukwa waige mfano huu kwenye utekelezaji miradi ya ujenzi ili kupunguza gharama za fedha za serikali “alisisitiza Mkirikiti.

Awali akitoa taarifa ya miradi, Mkuu wa Gereza la Kilimo Mollo Mrakibu wa Magereza (SP) Nicostratus Magori alisema mradi wa nyumba za kuishi askari umetekelezwa kwa lengo la kupunguza uhaba wa makazi bora ya askari .

Aliongeza kusema gharama halisi za mradi wa nyumba hiyo ni shilingi Milioni 55 ambapo gereza kupitia miradi yake limechangia shilingi Milioni 17.3 na Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) alichangia shilingi Milioni 38

Kuhusu mradi wa maji safi na salama SP Magori alisema jumla ya shilingi Milioni 7.6 imetumika kufufua mradi huo ambapo fedha zote zimetokana na miradi ya gereza Mollo.

SP Magori alitoa ombi kwa Mkuu wa Mkoa kuwa gereza lisaidie kupata miradi mbalimbali kwa lina nguvu kazi na utaalam hatua itakayosaidia kutekeleza miradi kwa ubora huku gereza likiongeza uwezo wake wa kujitegemea kimapato.

“Miradi hii licha ya kutuimarisha kiuchumi, inasaidia pia kutoa mafunzo ya ujuzi kwa wafungwa ili watakapomaliza vifungo vyao itawasaidia kuwa raia wema kwa kufanya kazi halali za kujitegemea” alisema SP Magori.

Gereza la Kilimo Mollo lilianzishwa mwaka 1967 ambapo lina eneo la ukubwa ekari 8,989 na kwa sasa lina miradi ya ujenzi wa nyumba ya kulala wageni, ujenzi wa bwalo, ujenzi wa fremu 11 za maduka na ujenzi wa viwanda vidogo vya kuchaka mazao ya ngano, alizeti na mahindi.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa