• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

“Halmashauri isiyopanda Miti Milioni 1.5 mwaka huu kutozwa faini,” RC Wangabo.

imewekwa Tar: January 20th, 2018

Rukwa Regional Commissioner Hon. Joachim Wangabo has instructed the four councils in Rukwa to make sure they reach the target of planting 1.5 million tree by the end of the year 2017/2018 so that to reach the target of the region of planting 6 million trees and failure to do so, a council will pay a Million to the winning Council. 

Amesema kuwa Halmashauri itakayoshindwa kufikia lengo itatakiwa kulipa faini ya shilingi Milioni 1 kuilipa Halmashauri itakayofika lengo ambapo Halmashauri Mshindi inategemewa kupata shilingi Milioni 3 na fedha hizo itapewa taasisi itakayopanda miti mingi kuliko taasisi nyingine ya serikali ndani ya Halmashauri iliyoshinda hasa mashule ili kuwafundisha wanafunzi umuhimu wa kupanda miti.

“Halmashauri ambayo haikufikia lengo imuume kutoa shilingi Milioni 1 kumlipa mwenzake, katika hizo Halmashauri 4, kwa maana mshindi atapata shilingi Milioni 3, lakini endapo Halmashauri zote zitafikia malengo nitazipa Halmashauri Shilingi Milioni 1, na hiyo fedha itakwenda kwenye taasisi iliyopanda miti mingi kuliko taasisi nyingine hasa mashule,” Mh. Wangabo alibainisha.

Ameongeza kuwa mwaka ujao wa 2018/2019 halmashauri itakayoshindwa kufikia lengo la kupanda miti Milioni 1.5 italipa faini ya shilingi Milioni 5 ili kila halmashauri iweze kufikia lengo na kutimiza maelekezo ya serikali na kuwaonya wote wenye tabia ya kuchoma misitu jambo linalokwamisha jitihada za kutunza mazingira.

Ameyasema hayo alipokuwa akizindua siku ya kupanda miti  Kimkoa tarehe 19.1.2018 iliyofanyika katika katika Shule ya Sekondari Matai, Wilaya ya kalambo ambapo miti 100 ilipandwa katika uwanja uliopewa jina la Msitu wa Wangabo kama kuunga mkono juhudi za Mh. Joachim Wangabo katika kuhakikisha kuwa Mkoa wa Rukwa haubaki kuwa jangwa hasa kwa kilimo kinachotegemea mvua.

Nae akisoma risala Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Julieth Binyura kabla ya kumkaribisha Mh. Wangabo alisema kuwa miongoni mwa mikakakti iliyowekwa na Wilaya hiyo ni kuhakikisha kila Kaya inapanda miti mitano na kuhakikisha kila shule inatenga eneo la kupanda miti ya matunda na mbao.

Pia alitumia nafasi hiyo kutoa takwimu za miti iliyopandwa na Wilaya hiyo, “kwa mwaka 2016/2017 miti 497,896 ilipandwa na kwa mwaka 2017/2018 mategemeo ya Wilaya ni kupanda miti Milioni 1.5 pamoja na changamoto za mifugo pamoja na wananchi kukosa hamasa ya kupanda miti tutahakikisha tunatoa elimu na kutenga bajeti kwaajili ya shughuli hiyo,” Alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule amesema kuwa mkakati wa Wilaya ni kuhakikisha kila mwanafunzi kwa shule za msingi na sekondari anapatiwa mti na uongozi wa shule autunze na ukivunwa asilimia 40 atapewa mwanafunzi na asilimia 60 itabaki shuleni.

Nazo taasisi mbalimbali za utunzaji wa mazingira wameahidi kushirikiana na Halmashauri katika kutoa elimu na kuwa na vijiji vya mfano ambavyo wanakijiji wanaweza kutoa ushuhuda juu ya elimu ya mti waliyoipata na faida mabazo zimepatikana kutokana na wingi wa miti watakayokuwa nayo katika vijiji.

 Kwa mwaka 2016/2017 Mkoa wa Rukwa ulipanda miti 2,489,296 ambayo ni sawa na asilimia 41.5 ya lengo na mwaka 2017/2018 hadi sasa Mkoa umepanda miti 2,173,649 ambayo ni sawa na asilimia 36.22.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa