• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Halmashauri Toeni Fedha za Lishe

imewekwa Tar: March 2nd, 2022

HALMASHAURI TOENI FEDHA KUTEKELEZA AFUA ZA LISHE- RC MKIRIKITI

Na .OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti amezionya halmashauri za mkoa huo kwa kutokutoa fedha za utekelezaji wa afua za lishe katika kipindi cha Octoba hadi Desemba 2021.

Ametoa onyo hilo jana (25.02.2022) wakati akiongoza kikao cha tathmini ya mkataba wa shughuli za lishe kipindi cha Julai hadi Desemba 2012 kilichofanyika mjini Sumbawanga ambapo halmashauri zote nne ziliripotiwa kutoa fedha za lishe asilimia 17.5 tu hatua inayokwamisha shughuli za lishe.

“Leo ndio siku ya mwisho nisisikie kuwa Afisa Lishe anasema hajapewa fedha za kutekeleza shughuli wakati mkoa bado una tatizo la udumavu na utapiamlo .Wakurugenzi nendeni mkabadilike .Suala la lishe ni agenda muhimu kwa uhai wa watu wetu” alisisitiza Mkirikiti.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Bonoface Kasululu ilionyesha kuwa halmashauri za Sumbawanga Manispaa, Sumbawanga Vijijini, Nkasi na Kalambo zimetoa asilimia 17 na kupelekea mkoa uwe kwenye rangi nyekundu.

Dkt. Kasululu aliongeza kusema matokeo ya ujumla yanaonesha kuwa mkoa wa Rukwa una wastani wa alama asilimia 87 ambapo kiasi hicho kimechangiwa na kutokutolewa kwa fedha za afua za lishe kwa upande wa halmashauri.

“Asilimia ya bajeti ya halmashauri iliyotumika kutekeleza shughuli za lishe kati ya iliyotengwa rangi nyekundu ni asilimia 17.5 kiashiria hiki kinaendelea kufanya vibaya zaidi ikilinganishwa na matokeo ya asilimia 54 kipidi cha mwaka 2020/2021” alieleza Dkt. Kasululu.

Taarifa ya tathmini kwa kiashiria cha asilimia ya fedha zilizotumika kwa shughuli za lishe katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2021 kwenye halmashauri na asilimia zake kwenye mabano Manispaa ya Sumbawanga (0.0), Sumbawanga DC (18.9), Nkasi DC (0.0) na Kalambo DC (47.7) hatua inayofanya mkoa kuwa na jumla ya asilimia 17.5

Mmoja wa Maafisa Lishe toka Halmashauri ambaye hatuka jina litajwe alisema “tumekuwa tukiandika madokezo kuomba fedha za shughuli za lishe lakini hatupatiwi bila kupewa sababu. Octoba –Desemba  2021 niliomba shilingi 800,000 lakini hadi leo sijajibiwa na kazi zimesimama” alisema mtaalam huyo.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Jukwaa la Lishe Tanzania (PANITA) Aron Isaack alisema licha ya mkoa wa Rukwa kushika nafasi ya 13 kati 26 mwaka 2020/21 bado kuna changamoto kubwa ya shughuli za lishe kutopewa kipaumbele hatua inayosababisha utapiamlo na udumavu kuendelea.

Isaack aliongeza kuwa kunahitajika utashi wa kisiasa ili kutekelezwa kwa mkataba wa lishe miongoni mwa viongozi na watendaji wa serikali wakiwemo Waganga Wakuu wa Wilaya za Rukwa.

“Tunaishukuru serikali kwa kusimamia suala la lishe hasa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 iliyotamka suala la lishe kupewa kipaumbele “alisema Isaack.

Kwa mujibu wa taarifa ya lishe iliyotolewa na Wizara ya Kilimo Desemba 2020 ilionesha kuwa mikoa inayoongoza kwa uzalishaji mazao ya chakula ndio ina kiwango kikubwa cha udumavu unaotokana na utapiamlo ikiwemo Rukwa (47.9), Njombe (53.6) na Iringa (47.1).

Mwisho.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa