• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Helium Yaibuka Kikao cha Bodi ya Barabara na kuibua gumzo.

imewekwa Tar: February 25th, 2021

Wajumbe wa Bodi ya Barabara Mkoani Rukwa wamesikitishwa na kitendo cha Wakala wa Barabara za Mijini na Vijini (TARURA) Pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD) kushindwa kuonyesha mpango wa kufungua barabara zinazoelekea ziwa Rukwa hasa katika maeneo ambayo utafiti unaonesha kuwa kuna gesi ya Helium inayoweza kuchimbwa.

Akiibua hoja hiyo katika kikao cha Bodi hiyo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Ya Wilaya ya Sumbawanga Mh. Apolinary Macheta alisema kuwa hapo awali katika bonde la Ziwa Rukwa kulikuwa na njia za kuelekea katika ziwa Rukwa lakini hivi sasa hakuna na hivyo kuiomba serikali kuona umuhimu wa kutenga bajeti kwaajili ya kuweka miundombinu Rafiki kwaajili ya kufika katika mradi huo wa helium.  

“Lakini Mheshimiwa Mwenyekiti ukiangalia kuanzia (Kijiji cha) Muze, Uzia – Kijiji kimoja kutoka Muze, kama nilivyosema zamani kulikuwa na njia magari yanaweza yakaingia huko ziwani, (lakini sasa) hakuna hata njia moja, hivyo nadhani jambo hili tulione kwa kina sana,” Alisema.

Akichangia hoja hiyo mbunge wa Nkasi Kaskazini Mh. Aida Khenan alisema kuwa haiwezekani kuifikia gesi hiyo endapo miundombinu sio rafiki na hivyo kutoa kutoa ushauri kwa TARURA juu ya kuweka vipaumbele vya ujenzi wa barabara ambazo zitachochea ukuaji wa uchumi wa Mkoa wa Rukwa.

“Tunazungumzia (mkoa) Songwe, wanaichukua hiyo fursa kwa maana gani, kama wameona sisi hatusemi lazima wafanye hivyo na mwisho wa siku wataanza kunufaika Songwe badala ya Rukwa, nilikuwa nashauri tena Pamoja na kwamba kuna brabara ambazo ni korofi sana, lakini lazima tuangalie kwanini tupeleke fedha pale, tunapeleka pale kwasababu barabara hii ikikamilika, vichocheo vya uchumi vinavyopita kwenye hii barabara vinaweza kutengeneza barabara nyingine,” Alisema.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kwela Mh. Deus Sangu alishauri bajeti ya TARURA kuwa na fungu la kuwezesha kujenga barabara zinazoelekea katika ziwa Rukwa kutokana na umuhimu na uharaka wake na kuiwasilisha Wizarani na hivyo ngazi ya mkoa kujivua lawama na kulibakisha mikononi mwa wizara husika na wenye maamuzi.

“Niwaombe TARURA mwaka huu wa fedha uwe ni mwaka wa mwisho kuwa na ‘Template’ ya aina hii (ya bajeti) tubadilishe mkafanye ‘survey’ mpya ya barabara, mje na mahitaji yaliyo halisi, tupeleke mahitaji yaliyo halisi siyo kukariri mambo ya miaka ya 2007 kwamaba milioni 600 ndio ‘Ceiling’ mwengine ana Shilingi bilioni 1.5 hatutafika,” Alieleza.

Katika kukazia hilo Mwenyekiti wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alisema kuwa Mkoa wa Rukwa umejaaliwa kuwa na rasilimali kubwa ya gesi ya Helium na endapo miundombinu ya kufikia gesi hiyo sio Rafiki, wawekezaji watashindwa kufika katika maeneo hayo.

“Ni lazima barabara hizi zipitike na kwa namna ile ni lazima zipate fedha za kutosha kutoka wizara inayohusika, vinginevyo tutakuwa tunazungumza tu ‘Helium gas’ umuhimu wake lakini hatuwezi kuichima ile gesi kwasababu ya barabara, kwahiyo ni lazima TANROAD na TARURA waongeze bajeti ya barabara zao, hususan kwenye bonde la ziwa Rukwa ili hiyo ‘Helium gas’ tuweze kuizungumzia vizuri katika kuichimba na kuitangaza, hatuwezi kuitangaza kama wawekezaji hawawezi kufika kwasababu ya kutokuwepo kwa barabara,” Alisisitiza.

Kwa mwaka wa fedha 2021/2022 TARURA wameomba kupitishiwa bajeti ya Shilingi 38,544,061,553.75 kwaajili ya matengenezo ya barabara ikijumuisha fedha za matengenezo Shilingi, 4,119,774,160.83 na Shilingi 34,424,287,392.92 kwaajili ya miradi ya maendeleo kwa barabara zenye urefu wa km 450.37 kwa matengenezo ya barabara na vivuko mchanganyiko 51.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa