• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Hoja za CAG zawaweka matatani watumishi watatu wa Halmashauri Wilaya ya Nkasi

imewekwa Tar: June 3rd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Nkasi kuwakamata watumishi watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kwa kula fedha zilizotokana na makusanyo ya Halmashauri na kujikopesha bila ya kuziwasilisha Benki na hatimae kuendelea kuibua hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali nchini (CAG).

Mh. Wangabo ameipa TAKUKURU siku saba kuhakikisha watumishi hao waliokula kiasi cha Shilingi 27,674,300/= wanarudisha fedha hizo na endapo watashindwa kufanya hivyo basi wafikishwe mahakamnami haraka iwezekanavyo na kuonya kuwa wadaiwa wa makusanyo ya halmashauri wamekuwa kama ugonjwa wa saratani uliokosa dawa huku Mkurugenzi na Madiwani wanaosimamia halmashauri hiyo wakishindwa kuwawajibisha.

“Nimeambiwa hizi fedha zinawahusu watumishi wa halmashauri watatu, mmoja anadaiwa milioni nane, na wengine wawili milioni tisa tisa, imesemwa tu wachukuliwe hatua za kisheria, lakininhaikutoa muda, hadi lini hawa watu wawe wamechukuliwa hatua hizo za kisheria, n ahata kwenye maeneo mengi hakuna muda wa kushughulikia hizi hoja kwamba kufikia tarehe Fulani hii iwe imekwisha, hakuna, sasa hawa watumishi watatu, TAKUKURU mko hapa, kamata hawa watumishi watatu, shughulikeni nao haraka iwezekanavyo kuanzia leo,” Alisema.

Pia ameeleza kuwa kwa mujibu wa taarifa za CAG kwa mwaka wa fedha 2018/2019, mapato yaliyokusanywa bila ya uthibitisho wa kupelekwa benki ni shilingi 47,725,415/= huku shilingi 20,051,115 zikiwa zimerudishwa, lakini wadaiwa hao hawajirekebishi na matokeo yake taarifa za mfumo wa ukusanyaji wa mapato hadi tarehe 31, Mei, 2020 unaonesha makusanyo ambayo hayajapelekwa benki kufikia Shililingi 53,813,308.38/= na hivyo kuiamrisha TAKUKURU kuwashughulikia.

Mh. Wangabo ametoa maelekezo hayo leo 3.6.2020 katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kuhusu utekelezaji wa hoja za Ukaguzi na Mapendekezo ya CAG ambapo pia amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha analipa madeni ya Madiwani ndani ya siku saba.

Mh. Wangabo amechukua hatua hizo ikiwa ni miongoni mwa utekelezaji wa maagizo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Mh. Suleiman Jafo ambaye hivi karibuni katika ziara yake mjini Sumbawanga alimtaka Mkuu huyo wa Mkoa kutumia vyombo alivyonavyo kushughulika na wadaiwa wa fedha za makusanyo ambazo hazikuwasilishwa Benki.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa