• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Hospitali za Wilaya 67 zafanyiwa tathmini juu ya maenedeleo ya ujenzi wake.

imewekwa Tar: December 19th, 2019

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamuhanga amesema kuwa  Ofisi ya Rais inaendelea kufanya tathmini kwa hospitali zote 67 kuhakikisha kwamba shilingi bilioni 100.5 ambazo zilitolewa kwa ujenzi wa hospitali hizo kuwa zimetumika vizuri.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imejenga hospitali 67 nchini na mkoa wa Rukwa umejengewa hospitali tatu za wilaya ambapo Mhandisi Nyamuhanga aliweza kutembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Kalamnbo, katika mji mdogo wa Matai iliyopokea shilingi Bilioni 1.5 lakini hakuridhishwa na ujenzi wa hospitali hiyo.

 “Kwa halmashauri ambazo fedha hizi zitakuwa hazijatumika vizuri kwakweli tutachukua hatua na katibu tawala wa mkoa kama nilivyoagiza jana, najua kuna vifaa ambavyo tayari vimeshanunuliwa pale ambavyo bado havijawekwa, havijajengwa kwa mfano maru maru na vifaa vingine uhakikishe kwamba kazi hiyo inaendelea ili vifaa hivyo vikishawekwa tuvitathmini sasa kiwango cha ukamilishaji wa hospitali ile ya halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kabla hatujafikiria kutoa fedha nyingine za kukamilisha,” Alisema.

Ameongeza kuwa halmashauri hiyo ya Kalambo imetaja mahitaji ya shilingi milioni 700 ili kuweza kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo jambo ambalo Mhandisi Nyamuhanga hakukubaliana nalo kutokana na tathmini iliyofanywa ya mahitaji ya fedha walizotoa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hizo kuwa yangebaki mambo machache ambayo yasingeweza kuzidi shilingi milioni 300 na kuongeza kuwa anahitaji maelezo ya ziada kutoka katika halmashauri hiyo ambayo hospitali yake imefikia ukamilifu wa asilimia 76 ambacho ni kiwango cha chini cha ukamilishaji.

Katika hatua nyingine amesema kuwa mwezi Aprili mwaka 2019 Ofisi ya Rais TAMISEMI ilitoa shilingi milioni 400 kwaajili ya upanuzi wa Zahanati ya Kijiji cha Samazi katika halmashauri ya Wilaya ya Kalambo ambapo zahanati hiyo inapandishwa hadhi na kuwa kituo cha Afya lakini amesikitishwa na malumbano yanayoendelea katika kijiji hicho juu ya eneo la ujenzi wa kituo hicho jambo lililopelekea kushindwa kuanza kwa ujenzi huo.

“Ofisi ya Rais TAMISEMI imetoa maelekezo kwamba upanuzi ufanyike katika eneo la zahanati iliyopo iongezewe majengo ili kiwe kituo cha afya cha Samazi kiweze kukamilika ili kiweze kufanya kazi, tusiendelee na malumbano tena tumeshatoa maamuzi kwamba upanuzi ufanyike pale kwenye zahanati ili tukipandishe hadhi ikiwe kituo cha afya, tunategemea kazi hiyo ianze mara moja na ikamilike ndani ya miezi mitatu,” Alisisitiza.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa