• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI RUKWA LAPOKEA MAGARI MATATU YA KISASA KUIMARISHA SHUGHULI ZA UOKOAJI

imewekwa Tar: October 27th, 2025


Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Rukwa limepatiwa magari matatu mapya ya kisasa kwa lengo la kuimarisha uwezo wake wa kukabiliana na majanga ya moto na kuimarisha huduma za uokoaji.

Uzinduzi wa magari hayo umefanywa na Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Charles Makongoro Nyerere leo Oktoba 27, 2025 katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.  


Kupatikana kwa magari hayo kunadhihirisha jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuboresha miundombinu na huduma za dharura nchini.

Serikali imeendelea kuimarisha sekta ya zimamoto na uokoaji kwa kuhakikisha vifaa vya kisasa vinapatikana, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kulinda maisha na mali za wananchi dhidi ya majanga mbalimbali.


Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza kasi na ufanisi katika kutoa huduma za dharura katika maeneo yote ya Mkoa wa Rukwa.


Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ameelekeza Halmashauri zote za Mkoa wa Rukwa kuhakikisha zinatenga maeneo maalum kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya kudumu vya zimamoto.  Aidha, ameagiza elimu ya kujikinga na majanga ya moto itolewe kwa wananchi kuhusu namna ya kuchukua tahadhari za mapema.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amelitaka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutumia magari hayo kwa uadilifu na akisisitiza matunzo bora.


Wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wameipongeza na kuishukuru Serikali kwa kuiimarisha Zimamoto mkoani Rukwa.


Kupatikana kwa magari mapya ya zimamoto kunatarajiwa kuongeza ufanisi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika Mkoa wa Rukwa, na hivyo kuboresha zaidi huduma za dharura na usalama wa wananchi kwa ujumla.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE( CSEE) 2025 January 31, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO SUMBAWANGA; ASISITIZA UMUHIMU WA HATI MILIKI ZA MAENEO YA TAASISI

    January 29, 2026
  • UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO; RC MAKONGORO AHIMIZA UBORA NA KUZINGATIWA KWA MUDA WA UTEKELEZAJI NKASI DC

    January 28, 2026
  • KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAIS SAMIA; RC MAKONGORO AMUUNGA MKONO KWA KUONGOZA WANANCHI RUKWA KUPANDA MITI 4565

    January 27, 2026
  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa