• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

JUMARU

imewekwa Tar: December 28th, 2021

MZEE KIMITI AWATAKA WANA RUKWA KUIUNGA MKONO SERIKALI

Waziri Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyehudumu tangu Awamu ya kwanza hadi ya tatu Paul Kimiti ametoa wito wa wananchi wa mkoa wa Rukwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali ili kusukuma agenda ya maendeleo Rukwa.

Mzee Paul Kimiti (81) ambaye amewahi kuhudumu kama Waziri, Mbunge na Mkuu wa Mkoa kwa nyakati tofauti ametoa rai hiyo (27.12.2021) mjini Sumbawanga wakati wa Mkutano Mkuu Maalum wa Jukwaa la Maendeleo Mkoa wa Rukwa (JUMARU).

“Tusipo isaidia serikali tutakaoumia ni sisi wananchi. Tuwasaidie viongozi wetu Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa wilaya watekeleze majukumu yao kwa ufanisi ili Rukwa ipige hatua za kimaendeleo” alisema Mzee Kimiti.

Aliongeza kusema JUMARU haipaswi kutumika kama jukwaa la kisiasa bali lengo lake liwe kuibua hoja na agenda za kuisaidia serikali kupanga mipango ya kiuchumi kwa maslahi ya wana Rukwa.

“Kaeni kama pete na kidole. JUMARU na serikali wafanye kazi kwa pamoja. Msigombane kwenye makundi ya whatsapp (mitandao ya kijamii) hayasaidii kuijenga Rukwa kimaendeleo” alisisitiza Mzee Kimiti.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti alieleza masuala manne muhimu kwa Jukwaa hilo kwanza , JUMARU kuibua hamasa ya maendeleo kwa kujenga ushawishi kwa wadau ili wachangie ukuaji uchumi wa Rukwa.

Jambo la pili, JUMARU iwatumie wazee maarufu na vijana wenye mawazo chanya kuweka mipango endelevu ya kufanya mkoa wa Rukwa upige kasi ikiwemo miradi ya maendeleo na tatu, jukwaa hilo litumike kupata agenda za kuiwezesha serikali kuchukua hatua za kusimamia maendeleo ya wananchi.

Mkirikiti alitaja jambo la nne kwa JUMARU kuwa ni kuhamasisha sekta ya michezo ili ichangie zaidi katika kuzalisha ajira hususan kwa vijana na kufanya mkoa wa Rukwa utambulike na kuchangia zaidi kwenye pato la taifa huku akitolea mfano uwepo wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania Prison na manufaa ya kiuchumi yanayopatikana Sumbawanga.

“Rukwa bado tupo nyuma kimaendeleo hivyo ni jukumu la JUMARU kushauri serikali namna gani ya kufanya kilimo kichangie zaidi kwenye uchumi na sekta zingine ikiwemo ushirika ambao una nafasi kubwa kuondoa unyonyaji kwa wakulima wadogo” alisema Mkirikiti.

Naye Mwenyekiti wa JUMARU Helena Khamsini alisema dira ya jukwaa hilo ni kuwa na Rukwa yenye maendeleo endelevu katika nyanja zote hususan elimu, afya, mazingira, uchumi na utamaduni.

Mkutano huo Maalum umehudhuriwa na Wazee maarufu, viongozi wa kimila, viongozi wastaafu wa serikali, vijana, wawakilishi wa akina mama na wasanii.

Mwisho.

Matangazo

  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Kodi kwa Maendeleo September 15, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chanjo Polio

    May 18, 2022
  • NFRA

    May 11, 2022
  • Vyama vya Ushirika

    May 05, 2022
  • Eng. Kundo: Nimeridhishwa na Zoezi la Anwani za Makazi Rukwa

    April 27, 2022
  • Angalia Zote

Video

RC Mkirikiti akabidhiwa Ofisi Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0764902066

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa