• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

JUMARU

imewekwa Tar: December 28th, 2021

MZEE KIMITI AWATAKA WANA RUKWA KUIUNGA MKONO SERIKALI

Waziri Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyehudumu tangu Awamu ya kwanza hadi ya tatu Paul Kimiti ametoa wito wa wananchi wa mkoa wa Rukwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali ili kusukuma agenda ya maendeleo Rukwa.

Mzee Paul Kimiti (81) ambaye amewahi kuhudumu kama Waziri, Mbunge na Mkuu wa Mkoa kwa nyakati tofauti ametoa rai hiyo (27.12.2021) mjini Sumbawanga wakati wa Mkutano Mkuu Maalum wa Jukwaa la Maendeleo Mkoa wa Rukwa (JUMARU).

“Tusipo isaidia serikali tutakaoumia ni sisi wananchi. Tuwasaidie viongozi wetu Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa wilaya watekeleze majukumu yao kwa ufanisi ili Rukwa ipige hatua za kimaendeleo” alisema Mzee Kimiti.

Aliongeza kusema JUMARU haipaswi kutumika kama jukwaa la kisiasa bali lengo lake liwe kuibua hoja na agenda za kuisaidia serikali kupanga mipango ya kiuchumi kwa maslahi ya wana Rukwa.

“Kaeni kama pete na kidole. JUMARU na serikali wafanye kazi kwa pamoja. Msigombane kwenye makundi ya whatsapp (mitandao ya kijamii) hayasaidii kuijenga Rukwa kimaendeleo” alisisitiza Mzee Kimiti.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti alieleza masuala manne muhimu kwa Jukwaa hilo kwanza , JUMARU kuibua hamasa ya maendeleo kwa kujenga ushawishi kwa wadau ili wachangie ukuaji uchumi wa Rukwa.

Jambo la pili, JUMARU iwatumie wazee maarufu na vijana wenye mawazo chanya kuweka mipango endelevu ya kufanya mkoa wa Rukwa upige kasi ikiwemo miradi ya maendeleo na tatu, jukwaa hilo litumike kupata agenda za kuiwezesha serikali kuchukua hatua za kusimamia maendeleo ya wananchi.

Mkirikiti alitaja jambo la nne kwa JUMARU kuwa ni kuhamasisha sekta ya michezo ili ichangie zaidi katika kuzalisha ajira hususan kwa vijana na kufanya mkoa wa Rukwa utambulike na kuchangia zaidi kwenye pato la taifa huku akitolea mfano uwepo wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania Prison na manufaa ya kiuchumi yanayopatikana Sumbawanga.

“Rukwa bado tupo nyuma kimaendeleo hivyo ni jukumu la JUMARU kushauri serikali namna gani ya kufanya kilimo kichangie zaidi kwenye uchumi na sekta zingine ikiwemo ushirika ambao una nafasi kubwa kuondoa unyonyaji kwa wakulima wadogo” alisema Mkirikiti.

Naye Mwenyekiti wa JUMARU Helena Khamsini alisema dira ya jukwaa hilo ni kuwa na Rukwa yenye maendeleo endelevu katika nyanja zote hususan elimu, afya, mazingira, uchumi na utamaduni.

Mkutano huo Maalum umehudhuriwa na Wazee maarufu, viongozi wa kimila, viongozi wastaafu wa serikali, vijana, wawakilishi wa akina mama na wasanii.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa