• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kamati ya watu wenye ulemavu Rukwa kutekeleza agizo la Waziri Mkuu.

imewekwa Tar: June 11th, 2018

Kamati ya watu wenye ulemavu Mkoa wa Rukwa imeaswa kuhakikisha inawatambua watu wenye ulemavu na kubaini mahitaji yao pamoja na kuona namna ya kutatua changamoto zao ili kuweza kuwasaidia katika kufikia malengo yao katika sekta mbalimbali za kimaendeleo.

“Katika Mkoa wa Rukwa tunachamoto kubwa juu ya namna ya kuwahudumia watu wenye ulemavu, kwani mara nyingi watu hawa wamekuwa wakileta malalamiko yao katika ofisi hii, hivyo uwepo wa kamati hii utapunguza sana changamoto wanazokabiliana nazo ndugu zetu hawa.”Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alipokuwa akizindua kamati ya watu wenye ulemavu ngazi ya Mkoa.

Ameongeza kuwa ni matumaini ya serikali kuwa kamati hiyo itazisimamia kamati zote zilizopo chini yake kuanzia ngazi ya halmashauri, mitaa na vijiji ili kujua idadi ya watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya kitongoji hadi kufikia ngazi ya halmashauri na kupeleka taarifa ya utekelezaji wa majukumu yao kwa Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Kwa upande wake akisoma taarifa ya kamati katibu wa kamati ya watu wenye ulemavu mkoa Godfrey Mapunda amezitaja changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kutokuwa na taarifa sahihi juu ya haki zao, kutokuwepo kwa miundombinu isiyozingatia hali za watu wenye ulemavu zinazowapelekea kushindwa kushiriki kwenye shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na Imani potofu kwa jamii inayowapelekea kushindwa kupata elimu na mahitaji muhimu.

Na kueleza majukumu ya kamati hiyo ikiwa ni pamoja na “Jukumu la kwanza itakuwa ni kutambua haki na uwezo wa watu walio na ulemavu katika mkoa lakini pia kuwasaidia watu wenye ulemavu na familia zao na kupanga mipango yenye ufanisi ili kupunguza umasikini kupitia shughuli za kujiingia kipato, kuratibu shughuli zote za watu wenye ulemavu katika mkoa, kulinda na kukuza ustawi wa watu wenye ulemavu katika Mkoa,” Alisema.

Hadi kamati hiyo inazinduliwa na Mkuu wa Mkoa asilimia 42 ya kamati za watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya Kijiji hadi halmashauri zilikuwa zimeshaundwa na walemavu 774 wamebanika huku maazimio ya kamati hiyo ikiwa ni kuhakikisha kamati zinaundwa kwa asilimia 100 na walemavu wote kutambulika na kuwa na takwimu sahihi ili kuweza kuwafikishia huduma stahiki.

Hii ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa alilolitoa alipohudhuria hafla ya chakula cha mchana kwa watu wenye ulemavu iliyoandaliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya IPP, Bw. Reginald Mengi kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee mapema mwezi wa pili mwaka 2018.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa