• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kampeni Upandaji Miti 10,000 Rukwa

imewekwa Tar: January 25th, 2022

 KAMPENI YA UPANDAJI MITI 10,000 YAZINDULIWA RUKWA

Na. OMM Rukwa

Mkoa wa Rukwa imezindua zoezi la upandaji miti kwa ajili ya kuhamasisha jamii kuutunza mazingira na kurejesha uoto wa asili ambapo jumla ya miti Elfu Kumi imepandwa katika wilaya ya Kalambo.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alizindua kampeni hiyo jana (24.01.2022) katika kijiji cha Sundu wilaya ya Kalambo ambapo taasisi za umma na sekta binafsi zimeshiriki kupanda miti pembezoni na bwawa la maji la Sundu.

Mkirikiti amewataka viongozi wa taasisi zote za umma na binafsi kuendelea kupanda miti kwenye maeneo ya makazi na maeneo yaliyotengwa ili Rukwa iondokane na uharibifu wa mazingira na kurejesha uoto wa asili hatua itakayosaidia kuwa na uhakika wa mvua.

“Tujipange kupanda miti ili tuweze kupata faida kwa mazingira yetu kuwa bora na kuwa na uhahika wa hali ya hewa nzuri itakayoruhusu mvua nyingi kunyesha katika mkoa wetu kwani tumeharibu mno mazingira” alisema Mkirikiti.

Katika zoezi hilo lililoratibiwa na shirika lisilo la Kiserikali la Rukwa Environmental Organisation (REMSO)la Sumbawanga ambapo kupitia Mkurugenzi wake Mzee Nkoswe Zenol Noel liliratibu upatikanaji miti kutoka Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) Shamba la Miti Mbizi.

Kabla ya zoezi la upandaji miti Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aligawa Hati Miliki za Kimila za ardhi 400 kwa wananchi ambazo zimegharimu shilingi Milioni 65 kwa wananchi vijiji vya Ilambila(100), Kifone (100), Kamawe (100) na Kalaela (100) vilivyopo wilaya ya Kalambo.

Awali mapema Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Seleman Jaffo alizungumza na wadau wa mazingira wa Mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga ambapo aliwaeleza kuwa serikali ipo kwenye kampeni ya kuhamasisha upandaji miti kwa wanafunzi kwenye shule za sekondari na taasisi.

Dkt. Jaffo alibainisha kuwa amefurahishwa kuona mkoa wa Rukwa ulivyojipanga kuutunza mazingira ambapo wadau na serikali wameungana kuhakikisha wanafikia lengo la kupanda miti 10,000 mwaka huu.

“Tulizindua kampeni Maalum ya upandaji miti kwa kila mwanafunzi ambapo kwa mujibu wa takwimu Tanzania kuna wanafunzi milioni 14.1 wa shule za sekondari hivyo kila mmoja kupanda mti tutakuwa na miti Milioni 14.1 na kwa wanafunzi wa vyuo vya kati wapo takribani 400,000 hivyo kila mmoja atashiriki hatua itakayowezsha nchi kupanda miti Milioni 14.5 mwaka huu” alisisitiza Dkt. Jaffo.

Dkt. Jaffo akiwa mkoani Rukwa alishiriki kupanda miti pamoja na wanafunzi wa shule za sekondari ya Wasichana Sumbawanga na shule ya sekondari Kantalamba ambapo alisisitiza kila kaya kupanda miti mitatu kuzunguka mazingira yake.

Kuhusu kivutio cha utalii cha maporomoko ya maji Kalambo, Waziri Jaffo alitaka hatua madhubuti kuchukuliwa ili kuutunza mazingira ya eneo hilo yadumu vizazi na vizazi.

“Kalambo Falls haiwezi kuwepo endapo hatutatunza mazingira yake ikiwemo vyanzo vya maji. Endeleeni kutoa elimu juu ya utunzaji wa mazingira kwa manufaa ya taifa” alisisitiza Dkt. Jaffo.

Mwisho

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa