• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

KAMPENI YA TOKOMEZA VIKOPE

imewekwa Tar: August 18th, 2021

KAMPENI YA TOKOMEZA VIKOPE KUWAFIKIA WATU 600 RUKWA

 

Serikali kwa kushirikiana na shirika la IMA World Health imezindua kampeni ya usawazishaji wa vikope kwa wananchi wenye matatizo ya macho kwenye wilaya za Sumbawanga na Kalambo mkoa wa Rukwa.


Uzinduzi wa kampeni hiyo unalenga kuwafikia wananchi zaidi ya Mia Sita (600) waliobainika kuwa na matatizo ya vikope (Trakoma) kufuatia utafiti uliofanywa na shirika la IMA World Health kwenye wilaya hizo ambapo huduma ya usawazishaji itafanyika kwa njia ya upasuaji mdogo.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo jana (18.08.2021) katika Kituo cha Afya Matai wilaya ya Kalambo, Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryoba aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alisema lengo ni kuwatibu wote wenye matatizo ya macho ili waone vizuri.


“Kuwa na tatizo la vikope siyo dhambi, ni ugonjwa kama yalivyo magonjwa mengine hivyo nawasihi wote wenye shida hii kujitokeza kwenye kampeni hii ili kupata huduma ya matibabu inayotolewa bure na shirika la IMA World Health” alisema Waryoba.


Mkuu huyo wa wilaya aliongeza kusema tatizo la vikope linatibika na kuwa wananchi hawana budi kujitokeza na kupata matibabu kwenye vituo vya afya ili wakipona waweze kuendelea kuona vizuri na kuendelea na maisha kawaida kwenye jamii.

Kwa upande wake Afisa Mratibu wa shirika la IMA World Health Dkt. William Hyera alisema mkoa wa Rukwa kufuatia utafiti umeonesha una wagonjwa zaidi ya 600 wenye matatizo ya vikope unaopelekea wasione vizuri hivyo kuhitaji matibabu.


“Kwa sasa wilaya ya Kalambo imekisiwa kuwa na wagonjwa 271 huku Sumbawanga ikiwa na wagonjwa 354 kwa hiyo kwa sasa tunatarajia kufanyia upasuaji  kwa wagonjwa takribani 600 ingawa bado kuna wilaya zingine bado hatujapewa kibali hivyo hatuwezi kuzungumzia ”, alisema Dkt. Hyera.

Aliongeza kusema utambuzi wa wagonjwa unafanywa kwa ushirikiano na wataalam wa afya waliopatiwa mafunzo kwenye ngazi za vijiji na kata ili kuwezesha wafikiwe na huduma ambapo mwitikio ni mkubwa .


Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu alisema ugonjwa wa vikope sasa ni moja ya magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele kama kichocho, matende (mabusha) ambayo yanasababishwa na minyoo hivyo serikali imedhamiria kuyapatia matibabu.

Dkt. Kasululu aliongeza kusema ugonjwa unaoitwa vikope au Trakoma unaathiri eneo la kope za macho hasa za juu hatua inayopelekea kope zitazame ndani na hatua inayoweza kusababisha upofu usipotibiwa mapema.


“Wagonjwa wenye matatizo haya msijifiche ndani nendeni kwenye vituo vya afya kupata huduma ili kuepuka madhara ya upofu na kuwa huduma ya matibabu inatolewa bure “alisisitiza Dkt. Kasululu.


Awali akitoa taarifa ya mkoa, Dkt. Kasululu alisema takwimu za wagonjwa wa vikope kwa mkoa wa Rukwa waliokuwa wamejitokeza zinaonesha kwenye mabano kuwa mwaka 2018 (27), mwaka 2019 (50) na hadi Juni 2021 (73) lakini takwimu za utafiti zinasema wanaweza kuwepo zaidi ya 1,000.

Kampeni hii yenye kauli mbiu “Epuka Upofu, Wahi Matibabu ya Kusawazisha Kope”itakamilika ifikapo mwezi Aprili mwaka 2022 kwa mkoa wa Rukwa.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa