• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kikao cha Wadau wa Elimu

imewekwa Tar: February 28th, 2022

SERIKALI IMEFANIKIWA KUBORESHA ELIMU RUKWA: RC MKIRIKITI

Na .OMM Rukwa

Mkoa wa Rukwa umefanikiwa kuwezesha wanafunzi 16,264 waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza mwaka 2022 kuripoti shuleni kati ya lengo la wanafunzi 20,324 waliochaguliwa baada ya kufaulu mtihani wa darasa la saba mwaka jana.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha wadau wa elimu leo (24.02.2022) mjini Sumbawanga, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti alisema mafanikio hayo yametokana na jitihada za serikali ya Awamu ya Sita kufanikisha ujenzi wa madarasa 259 katika shule za sekondari chini ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa na Mapambano dhidi ya Uviko-19.

“Wanafunzi wa kidato cha kwanza walioripoti hadi kufikia tarehe 22 Februari, 2022 ni 16,264 sawa na asilimia 80.2 ya wanafunzi 20,324 waliochaguliwa. Na uandikishwaji wa wanafunzi wa darasa la elimu ya awali umefikia asimilia 90.4 baada ya wanafunzi 36,640 kuandikishwa kati ya wanafunzi 42,702 waliotarajiwa katika mkoa wa Rukwa” alisema Mkirikiti.

Mkirikiti aliwataka wadau hao wa elimu kuweka mikakati ya kujua watoto 4,060 ambapo hawajaripoti kidato cha kwanza wako wapi kwani serikali imeweka mazingira mazuri ikiwemo utoaji elimu bila malipo kwa elimu msingi.

Mkirikiti alitoa agizo kwa wadau wa elimu kufanya kazi ya kujua wanafunzi wenye mahitaji maalum walipo na ikiwemo sababu gani wengine hawajaandikishwa shuleni pia wakuu wa shule za sekondari za bweni kusimamia nidhamu za wanafunzi.

“Natoa wito kwa wakuu wa shule zenye hosteli wa mabweni kudhibiti mienendo na maadili ya watoto .Zipo dalili kuwa baadhi mienendo yao siyo mizuri” alionya Mkirikiti.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa mkoa alitoa pongezi kwa serikali ya awamu ya sita kwa kuupatia mkoa huo shilingi Bilioni 6.6 chini ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19 zilizotumika kujenga vyumba vya madarasa 259 shule za sekondari na madarasa 73 kwa vituo shikizi vya shule za msingi.

“Tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha zilizowesha kujengwa miundombinu ya madarasa mapya yaliyowezesha wanafunzi wote waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka huu 2022 kuripoti vema shuleni” alisisitiza Mkirikiti.

Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu akizungumza kwenye kikao hicho cha wadau wa elimu alisema lengo lake ni kufanya tathmini ya hali ya elimu kwa kuangalia mafanikio yaliyopatikana na namna ya kuboresha sekta ya elimu.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa