• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kikongwe kupatiwa kiwanja karibu na Ikulu ndogo halmashauri ya Nkasi.

imewekwa Tar: September 15th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kumtafutia kiwanja cha nyumba Bibi Georgina Kapilima ili waweze kujenga nyumba na kuishi bila ya bughudha.

Ushauri huo umetolewa baada ya bibi huyo kumuomba Mkuu wa Mkoa katika siku maalum ambayo Mkuu wa Mkoa aliiweka maalum kwaajili ya kusikiliza kero na maombi mbalimbali ya wananchi ambao walijitokeza kuzungumza moja kwa moja na Mkuu huyo.

Bibi huyo ambaye alianza kwa kuilaumu Halmashauri hiyo baada ya kufika katika ofisi hizo mara kadhaa akidai kutafutiwa kiwanja cha kununua baada ya kuona majumba yakiendelea kujengwa katika mji huo unaoendelea nae akiumia kwa kulipa kodi ya shilingi 45,000 kwa miezi mitatu, jambo ambalo linamuweka katika wakati mgumu kutafuta pesa ya kodi hiyo.

“Ombi la huyu bibi ni la msingi sana, maana kila kukicha anaona nyumba zinamea tu lakini yeye akihitaji kiwanja anaambiwa hakuna jambo ambalo halimuingii akilini, kwahiyo Mkurugenzi, na Katibu tawala fanyeni utaratibu huyu bibi apatiwe kiwanja aweze kujenga nyumba,” Mh. Zelote alieleza.

Awali alipokaribishwa kueleza shida yake mbele ya Mkuu wa MKoa Bibi Kapilima mwenye miaka 60 alisema kuwa kila akifika ofisi za halmashauri kuomba kiwanja anaambiwa hakuna huku akiona watumishi wa halmashauri hiyo wakiendelea kujenga majumba na kuongeza kuwa hataki kiwanja hicho bure na kuwa yupo tayari kukilipia ili nae awe na kwake.   

Kwa kulipatia ufumbuzi jambo hilo katibu tawala wa Wilaya ya Nkasi Festo Chonya alitoa ahadi ya kumpatia kikongwe huyo moja ya viwanja 35 vilivyopo karibu na ikulu ndogo ya Wilaya ya Nkasi, Mjini Namanyere.

Mbali na kikongwe huyo Mh. Zelote alisikiliza kero za wananchi 14 kwa siku hiyo na kuweza kuzipatia ufumbuzi na wananchi hao kuondoka wakiwa wameridhika na maamuzi ya Mkuu wa Mkoa katika kutatua kero zao hizo.

Katika kusikiliza kero hizo Mkuu wa mkoa alikuwa na wakuu wa Idara za halmashauri hiyo, wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa Wilay pamoja na baadhi wa wakuu wa idara kutoka katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa