• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE ATAKA MKAZO ELIMU YA LISHE RUKWA

imewekwa Tar: September 8th, 2024



Nkasi, Rukwa –


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2024, Ndg. Godfrey Mnzava, amewataka Maafisa Lishe mkoani Rukwa kuongeza mkazo wa utoaji wa elimu ya lishe kwa wananchi.


Agizo hilo limetolewa leo Septemba 8, 2024 katika kijiji cha Kantawa, wilayani Nkasi, wakati wa ukaguzi wa shughuli za Maadhimisho ya Siku ya Lishe.


Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 amesisitiza kuwa uhamasishaji wa lishe bora kwa wananchi vijijini ni muhimu ili kupunguza kiwango cha udumavu kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.


Naye Afisa Lishe wa Wilaya ya Nkasi ameeleza kuwa udumavu ni changamoto inayotokana na ukosefu wa uelewa wa kutosha kuhusu lishe bora miongoni mwa wananchi na kwamba Wilaya ya Nkasi imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha elimu inafika kwa wananchi.


Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa takribani nusu ya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano mkoani Rukwa wanakabiliwa na tatizo la udumavu huku kiwango cha udumavu kikitajwa kufikia asilimia 49.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 ametoa wito kwa Serikali za Mitaa kushirikiana na maafisa lishe na mashirika mbalimbali kuhakikisha elimu ya lishe inawafikia wananchi kwa ufanisi ili kupunguza tatizo la udumavu.


Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 zimeingia siku yake ya 4 Mkoani Rukwa. Awali Mwenge wa Uhuru ulikimbizwa katika Halmashauri za Wilaya ya Sumbawanga, Kalambo, Manispaa ya Sumbawanga kabla ya kuingia Nkasi.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa