• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA ASISITIZA UTUNZAJI WA MAZINGIRA SUMBAWANGA

imewekwa Tar: September 7th, 2024



Sumbawanga, 07 Septemba 2024 –


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Godfrey Mnzava, ameihimiza jamii ya Sumbawanga na mkoa wa Rukwa kwa ujumla kuchukua hatua madhubuti za kulinda mazingira kupitia zoezi la upandaji miti. Wito huo umetolewa wakati wa ziara ya Mwenge wa Uhuru katika Msitu wa Hifadhi ya Mbizi, ambapo zaidi ya shilingi milioni 137 zimetumika kuanzisha vitalu vya miti vinavyotarajiwa kutoa miti itakayopandwa na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kuboresha mazingira.


Akizungumza katika eneo la vitalu hivyo, Mhifadhi Mkuu wa Msitu wa Mbizi, Ignas Lupala, alieleza kuwa lengo la mradi huo ni kuwekeza katika uhifadhi wa mazingira kwa kupitia upandaji wa miti unaolenga kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Mradi huo pia unalenga kuwahusisha wananchi wa maeneo jirani kwa manufaa ya kijamii na kiuchumi.


Kwa upande wake, Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Godfrey Mnzava, amewataka wananchi wa Rukwa na Tanzania kwa ujumla kutambua umuhimu wa upandaji miti na uhifadhi wa mazingira. “Kila mmoja wetu ana jukumu la kuhakikisha kuwa mazingira yanatunzwa kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho, na upandaji miti ni njia moja wapo ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi,” alisema Mnzava.


Wananchi wanaozunguka Msitu wa Mbizi pia wameeleza jinsi wanavyonufaika na msitu huo, wakisisitiza kuwa upandaji miti na utunzaji wa mazingira unatoa fursa za kiuchumi na kijamii kwa jamii nzima.


Jumla ya miradi 11 yenye thamani ya shilingi bilioni 10.8 imekaguliwa ,kuwekewa jiwe la msingi na kuzinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024.

Matangazo

  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MBIO ZA MWENGE ZAENDELEA KALAMBO RUKWA, MIRADI YA MAENDELEO YAENDELEA KUMULIKWa

    September 30, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MANISPAA YA SUMBAWANGA, MIRADI YA BILIONI 30.3

    September 29, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA AMALI WILAYANI NKASI; KIONGOZI ATAKA WANANCHI WATUMIE FURSA YA ELIMU YA UFUNDI

    September 28, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MKOANI RUKWA; KUKIMBIZWA KWA SIKU NNE; KUMULIKA MIRADI YA BILIONI 55.3

    September 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa