• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

“Kwa gharama yoyote ile michezo lazima ikue Rukwa” RAS Rukwa.

imewekwa Tar: October 10th, 2017

Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bernard Makali ameahidi kusimamia michezo katika Mkoa wa Rukwa na kuhakikisha Mkoa haubaki nyuma katika mashindano mbalimbali ya kitaifa ikiwemo ligi kuu ya soka Tanzania bara

Bernard Makali ambaye pia ni Mwenhyekiti wa baraza la Michezo la Mkoa amesema kuwa michezo yote itasimamiwa kuanzia ngazi ya mtaa, kata na wilaya na kuwashirikisha wadau wote kuanzia mwananchi wa kawaida, madiwani, wabunge na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali zilizopo katika mkoa ili kusukuma maendeleo ya michezo katika Mkoa.

“Michezo yote itasimamiwa, siyo mpira peke yake, lazima wadau wote washirikishwe katika mkoa ili kukuza michezo katika mkoa wetu, kuna mama hapa amelalamika wanawake hawachezi, lakini kuna chama cha netiboli tumekiwezesha kwenda Dodoma kwenye uchaguzi wao na wamefanikiwa, hivyo wote wanawake kwa wanaume watashiriki kwenye michezo,” Makali alisisitiza

Aliyaongea maneno hayo alipoitisha kikao cha wadau wa michezo wa mkoa kabla ya kukabidhi mipira 100 iliyotolewa na chama cha mpira wa miguu taifa (TFF) kwa vilabu 20 vya watoto vilivyopo katika Mkoa wa Rukwa.

Pia aliviagiza vilabu vyote na viongozi wa vyama mbalimbali vya michezo waliohudhuria kikao hicho kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kutekeleza agizo la Makamu wa Rais wa Nchi mama Samia Suluhu la kufanya mazoezi kila jumamosi ya pili ya mwezi ili kuhamasisha michezo pamoja na kuimarisha afya za wanarukwa.

“Mkoa huu hatuhamasishi wananchi kufanya mazoezi katika jumamosi ya pili ya mwezi, sasa naagiza sisi tuliopo ndani hapa tuwahamasishe wananchi huko tunapoishi kufanya mazoezi, na nataka kuona ratiba ya kila kilabu kujua wanapofanyia mazoezi kila siku hna hasa jumamosi ya pili ya mwezi,” Alimalizia.

Katika kikao hicho wadau hao walielezea changamoto mbali mbali za michezo mkoani Rukwa ikiwemo kutokuwa na ushirikiano kati ya chama cah mpira cha Mkoa pamoja na vyama vya mpira vya Wilaya jambo linalopelekea kudhoofisha maendeleo ya mpira katika mkoa.

Akizungumzia migogoro iliyopo katika vyama hivyo na namna wanavyoendelea kuitafutia ufumbuzi Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Rukwa (RUREFA) Bw. Blas Kiondo amesema kuwa tangu aingie madarakani mwaka 2013 amekuwa akikabiliana na changamoto hiyo na kuahidi kuimaliza kabisa.

Kwa upande wake Afisa michezo wa Mkoa Gabrieli Hokororo ametahadharisha kuwa si vyema kuyafufua makovu na badala yake wadau waungane pamoja ili kupeleka maendeleo ya michezo mbele na hatimae Mkoa wa Rukwa usikike kwenye ramani ya michezo katika taifa.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa