• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Maandalizi ya Sensa Rukwa

imewekwa Tar: July 8th, 2022

ZOEZI LA SENSA SI LA KISIASA BALI KISHERIA- RC MKIRIKITI

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti amewataka wajumbe wa kamati ya sensa ya mkoa kuhakikisha wananchi wengi wakiwemo wenye ulemavu wanapata elimu ya sensa na kuwa tayari kuhesabiwa ifikapo Agosti 23 mwaka huu.

Ametoa kauli hiyo leo (07.07.2022) mjini Sumbawanga wakati wa kikao cha kwanza cha kamati ya sensa ya mkoa kilicholenga kutoa elimu na hamasa kwa wajumbe kujua majukumu yao ikiwemo hatua iliyofikiwa kwenye maandalizi ngazi ya mkoa.

“Katika jambo hili la sensa hakuna kuchelewa, kazi ya hamasa na elimu kwa wananchi itolewe kwa usahihi na kwa wakati ikiwemo kwa watu wenye ulemavu kote ndani ya halmashauri za mkoa wa Rukwa “alisema Mkirikiti.

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe wa kamati ya amani na viongozi wa mila , Mkirikiti aliongeza kusema kila mmoja mahala alipo awe na utaratibu wa kutamka neno sensa hatua itakayoongeza hamasa ya wananchi kutambua umuhimu wa kujiandaa kushiriki kwenye zoezi la sensa.

Mkirikiti alibainisha kuwa zoezi la sensa si la kisiasa bali ni la kisheria kwani taifa linalenga kupata takwimu na taarifa sahihi za watu wake kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo.

“Zoezi hili la sensa si la kisiasa bali la kisheria kwani serikali inalenga kujua idadi sahihi ya wake kwa ajili ya kuwa na mipango sahihi ya maendeleo" alisisitiza Mkirikiti.

Kwa upande wake Mchungaji Emmanuel Sikazwe ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Amani Mkoa wa Rukwa aliomba kuwepo na utaratibu mzuri wa kufikisha taarifa kuhusu sensa kwa wananchi ili kujenga uelewa mzuri hatua itakayoongeza tija kwenye zoezi la sensa.

Naye Katibu wa Bakwata Mkoa wa Rukwa Ustadh Mohamed Adam alishauri serikali kutoa nafasi ya kutosha kwa viongozi wa madhehebu ya dini kupata elimu ya kina kuhusu sensa ili wapate uelewa wa kuhamasisha jamii kujitokeza kushiriki kikamilifu kuhesabiwa ifikapo Agosti 23 mwaka huu.

“Tunahitaji muda wataalam watupe elimu ya nini maana ya sensa kwani hadi muda huu bado ujumbe wa sensa haujafahamika vizuri katika jamii yetu" alisema Ustadh Adam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mratibu wa Sensa Mkoa wa Rukwa Adam Ramadhan alisema tayari maeneo ya kuhesabia watu (EAs) 2,190 katika halmashauri zote nne za Rukwa yametengwa pamoja kazi ya kusambaza viperushi imefanyika.

Ramadhan alitaja idadi ya maeneo ya kuhesabia watu kwa kila halmashauri yaliyoandaliwa kuwa Sumbawanga Vijijini (494), Manispaa ya Sumbawanga (534), Kalambo (422) na Nkasi (740).

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa