• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Maandalizi ya Sensa Rukwa

imewekwa Tar: July 8th, 2022

ZOEZI LA SENSA SI LA KISIASA BALI KISHERIA- RC MKIRIKITI

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti amewataka wajumbe wa kamati ya sensa ya mkoa kuhakikisha wananchi wengi wakiwemo wenye ulemavu wanapata elimu ya sensa na kuwa tayari kuhesabiwa ifikapo Agosti 23 mwaka huu.

Ametoa kauli hiyo leo (07.07.2022) mjini Sumbawanga wakati wa kikao cha kwanza cha kamati ya sensa ya mkoa kilicholenga kutoa elimu na hamasa kwa wajumbe kujua majukumu yao ikiwemo hatua iliyofikiwa kwenye maandalizi ngazi ya mkoa.

“Katika jambo hili la sensa hakuna kuchelewa, kazi ya hamasa na elimu kwa wananchi itolewe kwa usahihi na kwa wakati ikiwemo kwa watu wenye ulemavu kote ndani ya halmashauri za mkoa wa Rukwa “alisema Mkirikiti.

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe wa kamati ya amani na viongozi wa mila , Mkirikiti aliongeza kusema kila mmoja mahala alipo awe na utaratibu wa kutamka neno sensa hatua itakayoongeza hamasa ya wananchi kutambua umuhimu wa kujiandaa kushiriki kwenye zoezi la sensa.

Mkirikiti alibainisha kuwa zoezi la sensa si la kisiasa bali ni la kisheria kwani taifa linalenga kupata takwimu na taarifa sahihi za watu wake kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo.

“Zoezi hili la sensa si la kisiasa bali la kisheria kwani serikali inalenga kujua idadi sahihi ya wake kwa ajili ya kuwa na mipango sahihi ya maendeleo" alisisitiza Mkirikiti.

Kwa upande wake Mchungaji Emmanuel Sikazwe ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Amani Mkoa wa Rukwa aliomba kuwepo na utaratibu mzuri wa kufikisha taarifa kuhusu sensa kwa wananchi ili kujenga uelewa mzuri hatua itakayoongeza tija kwenye zoezi la sensa.

Naye Katibu wa Bakwata Mkoa wa Rukwa Ustadh Mohamed Adam alishauri serikali kutoa nafasi ya kutosha kwa viongozi wa madhehebu ya dini kupata elimu ya kina kuhusu sensa ili wapate uelewa wa kuhamasisha jamii kujitokeza kushiriki kikamilifu kuhesabiwa ifikapo Agosti 23 mwaka huu.

“Tunahitaji muda wataalam watupe elimu ya nini maana ya sensa kwani hadi muda huu bado ujumbe wa sensa haujafahamika vizuri katika jamii yetu" alisema Ustadh Adam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mratibu wa Sensa Mkoa wa Rukwa Adam Ramadhan alisema tayari maeneo ya kuhesabia watu (EAs) 2,190 katika halmashauri zote nne za Rukwa yametengwa pamoja kazi ya kusambaza viperushi imefanyika.

Ramadhan alitaja idadi ya maeneo ya kuhesabia watu kwa kila halmashauri yaliyoandaliwa kuwa Sumbawanga Vijijini (494), Manispaa ya Sumbawanga (534), Kalambo (422) na Nkasi (740).

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa