• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Madiwani watakiwa kukabiliana na Mimba za Utotoni kwa kushirikisha wananchi kuimarisha Miundombinu ya Elimu

imewekwa Tar: December 17th, 2020

Baraza jipya la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa wametakiwa kukahikisha kila Kijiji na Kata katika maeneo yao kunakuwa na shule za Msingi na Sekondari ili kuwaepusha Watoto kutembea umbali mrefu kufuata elimu na hivyo kukutana na vikwazo vingi hali inayowapelekea wengine kushindwa kukamilisha masomo yao na kuishia kuolewa ama kupata mimba. 

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo terehe 15.12.2020 alipokuwa akitoa nasaha zake baada ya madiwani wa Baraza hilo jipya la Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kumaliza kula viapo vyao mbele ya wananchi waliohudhuria tukio hilo.

Wakati akielezea hali ya miundombuni ya elimu katika halmshauri hiyo Mh. Wangabo alisema kuwa Halmashauri hiyo yenye Vijiji 90 inatakiwa kuwa na Shule 90 za Msingi lakini kinyume chake ni vijiji 74 pekee ndio vyenye shule hizo huku vijiji 16 vikiwa havina shule za Msingi.

Na kuongeza kuwa Kata 21 pekee kati ya Kata 28 za Halmshauri hiyo ndio zenye Shule ya Sekondari na hivyo kuziacha Kata 7 zikiwa hazina Shule ya Sekondari jambo linalowasababisha wanafunzi kutembea umbali mrefu huku wakiwa hatarini kukumbana na wasiopenda maendeleo ya elimu kwa Watoto wakiwasuburi kuwatia mimba na hivyo kuwataka Madiwani kushirikiana na wananchi kutatua changamoto hiyo.

Aidha aliupongeza uongozi wa Wilaya ya Nkasi kwa kuweza kuwa na madarasa ya kutosheleza wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza kwa mwaka 2021 na kuwasisitiza kuendelea kutengeneza madawati na viti vya kutosha kwaajili ya wanafunzi hao.

“Nendeni mkasimamie kata zenu ziwe na shule za Sekondari, hizi kata saba ziwe na shule zake za Sekondari, Sasa hivi tunahangaika Mh. DC amesema hapa, kuhakikisha kwamba wanafunzi wote waliofaulu wanakwenda Sekondari, ninyi hapa nawapongeza hakuna tatizo hilo kwa upande wa wanafunzi waliochaguli kwenda kidato cha kwanza wakakosa nafasi, mko vizuri, ila mkaangalie suala la madawati na viti na kukamilisha vyumba ambavyo mshaanza kuvijenga,” Alisema.

“Na pale ambapo kuna Sekondari hakuna bweni, kajengeni bweni ili Watoto wa mbali na wenyewe wapate mahali pa kuishi salama, huko kwenye vijumba vya kupanga si salama, mtoto unampeleka akiwa vizuri anakurudishia mimba kisa ni mazingira haya ya kutolea elimu sio mazuri, chukueni hili mkalifanyie kazi,” Alisisitiza.

Akielezea Mkakati wa Wilaya kuhusu kuhakikisha kila mwanafunzi aliyechaguliwa kuingia kidato cha kwanza anakaa kwenye dawati Mkuu wa Wilaya ya Nkasi mh. Said Mtanda alisema kuwa watendaji wa halmashauri hiyo watafanya ziara katika shule zote za sekondari ili kuhakikisha wanafunzi hao wanakaa kwenye madawati.

“Kwahiyo watendaji wa Halmashauri tumekubaliana utekelezaji tarehe 28.1.2021. atakayeshindwa kwenda na kasi ya utekelezaji wa mipango hiyo tumekubaliana kama ni mratibu wa elimu ya Kata na kata yake haina madawati kitakachofuata ni tutafute mbadala wake naye tumtafutie shule akafundishe kwasababu hatuna njia nyingine kwa sasa, hatuwezi kuendelea na mwendo wa kubembelezana kwenye maendeleo,” Alisema.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa